-
Omar Sahabou: Imarati ina woga wa wimbi la demokrasia
Jul 06, 2019 21:53Mwanasiasa mashuhuri wa Tunisia kutoka chama cha Nidaa Tunis amesema kuwa serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu ina woga wa kupenya demokrasia na kuingia nchini humo; kwa sababu hiyo inafanya jitihada za kuangamiza demokrasia nchini Tunisia.
-
Imarati yaondoa idadi kubwa ya askari wake kutoka Yemen
Jun 28, 2019 23:30Umoja wa Falme za Kiarabu umewaondosha nchini Yemen idadi kubwa ya wanajeshi wake.
-
Balozi wa Imarati Tehran aitwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran
Jun 22, 2019 22:58Baada ya ndege ya Marekani kuingia katika anga ya Iran na kufanya ujasusi ikitokea katika kambi moja ya kijeshi ya Marekani huko Imarati, balozi mdogo wa Umoja wa Falme za Kiarabu hapa Tehran ameitwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ili kukabidhiwa malalamiko ya Tehran juu ya kwa nini Abu Dhabi inaruhusu ardhi yake kutumiwa kufanya ujasusi dhidi ya majirani zake.
-
Baada ya vitisho vya Answarullah, Imarati yaondoa vifaru vyake kusini mwa Yemen
Jun 22, 2019 07:36Habari kutoka nchini Yemen zinasema kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ambayo ni mmoja wa wavamizi wakuu wa ardhi ya Yemen umeondoa vifaru vyake 20 katika mji wa Aden wa kuisni mwa Yemen.
-
Qatar yasisitiza kuwa sera za Saudia ni haribifu katika eneo la Asia Magharibi
Jun 12, 2019 03:38Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim Al Thani, Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar akiwa safarini nchini Uingereza amesema: "Saudi Arabia ni nguvu ya uharibifu katika eneo lote la Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) na Afrika."
-
Zarif: Imarati inajaribu kuwa Israel ya pili katika Mashariki ya Kati
Jun 12, 2019 03:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema katika mahojiano na televisheni ya al Arabi kuwa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) unatumia mabilioni ya dola kununua silaha huku ukifanya jitihada za kujaribu kuwa Israel ya pili katika eneo.
-
Qatar: Saudia na Imarati zinachochea ugaidi na taharuki katika eneo
Jun 10, 2019 03:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, Mohammed bin Abdulrahman Aal Thani amesema sera za Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabi zinashadidisha ugaidi na kuchochea taharuki katika eneo la Asia Magharibi na barani Afrika.
-
Uchochezi wa Saudi Arabia na Imarati katika mgogoro wa Sudan
Jun 09, 2019 02:50Mgogoro wa kisiasa nchini Sudan ulishadidi Juni 3 baada ya wanajeshi kuwashambulia waandamanaji waliokuwa wamekusanyija nje ya makao makuu ya jeshi ambapo raia zaidi ya 100 waliuawa katika vurumai hiyo.
-
Mamluki wa Imarati washambulia msikiti Yemen na kuua watu kadhaa
Jun 08, 2019 07:07Mamluki wa Umoja wa Falme za Kiarabu ambao ni sehemu ya muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia wamevamia msikiti mmoja katika mkoa wa Dhale kusini mwa Yemen na kuua watu sita waliokuwa kwenye nyumba hiyo ya ibada, mbali na kuwateka nyara wengine wanne.
-
Zarif aikosoa Mossad ya Israel kwa kuituhumu Iran kwa ulipuaji wa meli za mafuta al-Fujairah, UAE
Jun 05, 2019 22:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepuuzilia mbali 'taarifa za kiintelijensia' za Shirika la Kijasusi la Utawala wa Kizayuni wa Israel Mossad zinazodai kwamba Iran imehusika na kulipuliwa meli za mafuta katika Bandari ya al-Fujairah huko Umoja wa Falme za Kiarabu, akisisitiza kuwa amewahi kutoa indhari huko nyuma kuhusu kupikwa njama za kutaka kuibua taharuki katika eneo.