-
Zohreh Elahian, mwanamke wa kwanza kujiandikisha kuwania urais Iran 2024
Jun 02, 2024 01:41Mbunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Zohreh Elahian amekuwa mwanamke wa kwanza kujiandikisha kugombea uchaguzi wa mapema wa duru ya 14 ya urais wa Jamhuri ya Kiislamu, kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raisi katika ajali ya helikopta.
-
Persepolis yatwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Iran
Jun 02, 2024 06:59Klabu ya Persepolis ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka hapa nchini baada ya kuichachafya klabu ya Mes Rafsanjan Jumamosi. Esteqlal imemaliza ya pili baada ya kuisasambua Peykan mabao 2-0.
-
Iran na Saudia zasisitiza kupanua na kustawisha uhusiano wao
May 31, 2024 22:51Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia wamesisitiza kustawishwa uhusiano wa pande mbili katika mazungumzo waliyofanya kwa njia ya simu.
-
Kaimu Rais wa Iran asisitiza kuhusu kuimarishwa uhusiano wa kibiashara wa Iran na Oman
May 28, 2024 00:54Kaimu Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameutaja uhusiano wa Iran na Oman kuwa wa kihistoria na wa kidugu na kusema: Iwapo uwezo uliopo utatumika vizuri, maingiliano ya kiuchumi na kibiashara kati ya Iran na Oman yataongezeka hadi mara kadhaa ya kiwango cha sasa.
-
Msemaji: Mazungumzo ya kuondoa vikwazo dhidi ya Iran yanaendelea
May 27, 2024 23:18Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa mazungumzo ya kuondoa vikwazo dhidi ya Tehran yanaendelea.
-
"Vitisho vya nyuklia vya Israel vitabadilisha mlingano wa usalama katika eneo"
May 26, 2024 22:50Katibu wa Baraza la Kistratajia la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesema vitisho vinavyotolewa na maafisa wa utawala wa Kizayuni wa Israel vya kutumia silaha za nyuklia huenda vikawalazimisha wengine kuangalia upya sera zao za nyuklia katika eneo la Asia Magharibi.
-
Ejei: Sera za ndani na nje za Iran zitaendelea kuwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali
May 26, 2024 03:53Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika mazungumzo na Mkuu wa Baraza Kuu la Mahakama la Iraq kuwa; Sera za ndani na nje za Iran zitaendelea kuimarika zaidi kuliko hapo awali.
-
Iran yapongeza maadhimisho ya "Siku ya Afrika"
May 26, 2024 03:41Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amepongeza na kutoa mkono wa kheri kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Afrika (Africa Day).
-
Watu milioni 3 washiriki mazishi ya Rais Ebrahim Raisi mjini Mashhad
May 23, 2024 10:14Waombolezaji zaidi ya milioni tatu wameshiriki katika mazishi ya kumuaga na Rais Ebrahim Raisi wa Iran, aliyekufa shahidi katika ajali ya helikopta iliyotokea Jumapili iliyopita katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.
-
Kaimu Rais: Iran itaendelea kuunga mkono kambi ya muqawama
May 23, 2024 07:32Kaimu Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kuunga mkono kikamilifu kambi ya muqawama.