-
Kipaumbele cha Iran ni usitishaji vita huko Gaza, utawala wa Israel utatiwa adabu
Aug 10, 2024 07:06Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu katika Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa, haki ya kujilinda kuhusiana na mauaji ya Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas mjini Tehran haina uhusiano wowote na usitishaji vita huko Gaza na kusema kuwa, usitishaji vita katika eneo la Magharibi mwa Asia ni kipaumbele cha Iran.
-
Iran: Israel imetengwa zaidi kisiasa duniani baada ya kumuua kigaidi Haniyah
Aug 09, 2024 03:50Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, kulaaniwa Israel kote duniani kwa mauaji ya Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas), Ismail Haniyah kumezidisha kutengwa kisiasa kwa utawala huo wa Kizayuni.
-
Kani: Iran haina mipaka katika kuimarisha uhusiano na Afrika
Aug 09, 2024 03:49Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu haina kikomo wala mipaka katika kuimarisha na kupanua uhusiano wake na nchi za bara Afrika.
-
Kikao cha OIC cha mjini Jeddah na majukumu ya nchi za Kiislamu
Aug 08, 2024 06:28Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imeamua kuitisha kikao dha dharura mjini Jeddah, Saudi Arabia wakati huu ambapo Iran na kambi ya muqawama inajiandaa kutoa majibu makali kwa Israel kutokana na vitendo vya kigaidi vya utawala wa Kizayuni.
-
Bagheri: Haturuhusu usalama wa kanda hii uchezewe na Israel
Aug 07, 2024 07:57Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria uamuzi wa Tehran wa kutekeleza hatua hahali, madhubuti na ya kuutia adabu utawala wa Kizayuni na kusisitiza kuwa: Iran haitaruhusu Israel ichezee usalama wa kanda hii kwa maslahi haramu ya genge la kigaidi linalotawala huko Tel Aviv.
-
Bagheri Kani: Iran itatoa jibu madhubuti kwa ugaidi wa Israel
Aug 07, 2024 03:36Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema utawala wa Israel ndio chanzo halisi cha ukosefu wa utulivu katika eneo la Asia Magharibi, na kwamba utawala huo wa Kizayuni unapata ujasiri wa kutenda jinai na vitendo vyake vya kigaidi kutokana na kimya cha nchi za Ulaya.
-
Mahakama: Iran itatumia uwezo wake wote kujibu mauaji ya Haniyah
Aug 06, 2024 22:58Msemaji wa Idara ya Mahakama ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itatumia uwezo wake wote kulipiza kisasi cha mauaji ya Ismail Haniyah, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS), akiwa mjini Tehran.
-
Iran na Russia katika mkondo wa kuimarisha ushirikiano
Aug 06, 2024 10:42Jumatatu ya jana tarehe 5 Agosti, Katibu wa Baraza la Usalama la Taifa la Shirikisho la Russia aliwasili mjini Tehran kwa lengo la kuimarisha maingiliano na kuchunguza masuala ya kieneo, kimataifa na uhusiano wa pande mbili.
-
Iran: Nchi za Magharibi zimepoteza utu na heshima katika vita vya Gaza
Aug 06, 2024 09:50Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, nchi za Magharibi zimepoteza utu na heshima yao katika vita dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza na zimekumbwa na mmomonyoko wa kimaadili na mporomoko wa ustaarabu.
-
Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Ni lazima tusimame dhidi ya utawala mshari wa Kizayuni
Aug 06, 2024 04:16Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Tehran inapaswa kusimama kidete kukabiliana na utawala muovu kwa jina la utawala wa Kizayuni, ambao ndio chanzo cha ukosefu wa amani katika eneo.