-
Iran: Hatubabaishwi na bwabwaja na matamshi ya vitisho ya Marekani
Jan 30, 2023 23:24Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imekosoa porojo na matamshi ya vitisho ya Marekani na kuonya kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itatoa jibu kali kwa hatua yoyote ya uvamizi dhidi ya taifa hili.
-
Iran yazima mashambulio ya droni katika mkoa wa Isfahan
Jan 29, 2023 09:13Wizara ya Ulinzi ya Iran imesema vyombo vya usalama vya Jamhuri ya Kiislamu vimefanikiwa kuzima mashambulio ya ndege zisizo na rubani (drone) dhidi ya kituo cha kijeshi katika mji wa Isfahan, katikati mwa nchi.
-
Jibu la Iran kwa vikwazo vya Umoja wa Ulaya
Jan 27, 2023 23:02Katika kukabiliana na vikwazo vya hivi karibuni vya Umoja wa Ulaya, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imechapisha orodha mpya ya shakhsia na taasisi za Ulaya ambazo zimewekewa vikwazo na serikali ya Tehran.
-
Iran na Tanzania zahimiza ushirikiano zaidi baina yao hasa katika uwekezaji viwandani
Jan 27, 2023 03:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Tuko tayari kutoa ujuzi na uzoefu wetu, hasa katika nyanja za elimu, kilimo, uvuvi, ujenzi wa mabwawa, usimamizi wa vyanzo vya maji na kilimo umwagiliaji, ili kuisaidia Tanzania katika juhudi zake za mapinduzi ya viwanda.
-
Gharibabadi: Magharibi inatumia suala la wanawake kuzishinikiza nchi huru
Jan 26, 2023 23:17Afisa wa ngazi ya juu wa haki za binadamu nchini Iran amesema nchi za Magharibi zinatumia suala la wanawake kuziweka chini ya mashinikizo nchi huru duniani.
-
Iran yasisitiza kukomeshwa chokochoko za utawala wa Kizayuni huko Syria
Jan 26, 2023 04:45Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa: Baraza la Usalama linapasa kuushinikiza utawala wa Kizayuni ili uhitimishe chokochoko na hatua zake za uvamizi dhidi ya mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi yote ya Syria.
-
Iran yajibu mapigo, yatangaza vikwazo dhidi ya EU, Uingereza
Jan 26, 2023 00:32Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imejibu hatua ya Umoja wa Ulaya na Uingereza ya kuwawekea vikwazo baadhi ya shakhsia binafsi na wa kiserikali wa Jamhuri ya Kiislamu, kwa kutangaza vikwazo dhidi ya shakhsia na taasisi za EU na Uingereza.
-
Raisi: Uhusiano wa Iran na Syria umejengeka katika misingi ya muqawama
Jan 24, 2023 23:34Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uhusiano wa Iran na Syria ni thabiti na kwamba umejengwa katika misingi ya moyo wa muqawama na mapambano ya wananchi wa mataifa haya mawili.
-
"Sweden haiwezi kuficha chuki zake dhidi ya Uislamu kwa barakoa ya uhuru"
Jan 24, 2023 23:00Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameashiria kitendo cha kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Sweden na kueleza kuwa, nchi hiyo ya Magharibi haiwezi kuficha chuki zake dhidi ya Uislamu kwa kutumia barakoa ya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni.
-
EU yaendeleza msimamo wa uhasama dhidi ya Iran
Jan 23, 2023 23:15Umoja wa Ulaya umeendeleza misimamo yake ya uhasama kwa Iran kwa kuiwekea vikwazo vipya.