-
Araqchi: Marekani inabeba dhima kwa hali ya sasa Afghanistan
Dec 05, 2021 23:46Katibu wa Baraza la Kistratajia la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesema Marekani ndiyo inayopaswa kulaumiwa na kuwabishwa kutokana na matatizo mengi yanaoikumba Afghanistan.
-
Iran: Hatutalegeza kamba katika kushinikiza kuondolewa vikwazo haramu
Dec 05, 2021 11:24Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya kisiasa amesema Jamhuri ya Kiislamu katu haitolegeza kamba katika mazungumzo ya Vienna, Austria na itaendelea kushinikiza kuondolewa vikwazo vya kidhalimu na vilivyo kinyume cha sheria vya Marekani dhidi ya taifa hili.
-
Borell na Abdullahiyan: Anga ya mazungumzo ya Vienna ni chanya
Dec 03, 2021 23:08Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran wamewasiliana kwa njia ya simu na kuyatathmini mazungumzo ya kuondoa vikwazo yanayoendelea mjini Vienna, Austria kuwa ni chanya.
-
Iran na Syria kuimarisha zaidi ushirikiano wao wa kiuchumi na kibiashara
Dec 03, 2021 07:19Waziri wa Uchumi wa Syria amesema kuwa, nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zina nia ya kweli ya kuimarisha zaidi na zaidi ushirikiano wao wa kiuchumi na kibiashara.
-
"Iran ni nguzo ya ulimwengu wa Kiislamu, kambi ya muqawama"
Dec 03, 2021 00:54Mkuu wa Utamaduni wa Harakati ya Kujitolea ya Wananchi wa Iraq maarufu kama Hashd al Sha'abi amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ndio nguzo ya ulimwengu wa Kiislamu na mrengo wa muqawama na mapambano ya Kiislamu.
-
Kuunga mkono kundi la 4+1 kuondolewa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran
Nov 30, 2021 23:10Sambamba na kuanza duru ya saba ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran na kundi la 4+1 huko Vienna Austria, kumeongezeka himaya na uungaji kwa takwa la haki na la kisheria la Iran la kuondolewa vikwazo vya upande mmoja ilivyowekewa kidhalimu na Marekani.
-
Mazungumzo ya Vienna, changamoto na matarajio
Nov 29, 2021 08:32Leo Novemba 29 mji mkuu wa Austria, Vienna ni mwenyeji wa mazungumzo baina ya Iran na nchi za kundi la 4+1 kuhusu kuondolewea vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran. Nchi za 4+1 ni China Russia, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani pamoja na mwakilishi wa Umoja wa Ulaya
-
Iran na Mali zatia saini mapatano ya ushirikiano katika madini
Nov 28, 2021 23:49Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Mali zimetiliana saini mapatano ya ushirikiano katika sekta ya uchimbaji madini. Mapatano hayo ni kati ya Shirika la Uhandisi wa Madini la Iran na Idara ya Uchimbaji Madini Mali.
-
Iran haitaki makubaliano ya muda, yataka vikwazo viondolewe kwa mkupuo
Nov 27, 2021 01:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, vikwazo vyote haramu vya Marekani dhidi ya taifa la Iran vinapaswa kuondolewa kwa mkupuo, na kwamba Tehran katu haitakubali 'makubaliano ya muda' kwenye mazungumzo ya Vienna ya kujadili makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, yanayoanza ndani ya siku chache zijazo.
-
Iran: Marekani haina chaguo jingine isipokuwa kukubali uhalisia wa mambo
Nov 23, 2021 04:03Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ambaye anaongoza timu ya mazungumzo ya Jamhuri ya Kiislamu na kundi la 4+1 yatakayoanza Novemba 29 huko Vienna amesema kuwa, Marekani sharti ikubali hali halisi ya mambo kwa kufungamana na ahadi ilizotoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA.