-
Rais Pezeshkian: Iran haifanyi mazungumzo iwe imezungumza tu, inataka tija inayoonekana
Feb 18, 2026 07:36Rais Masoud Pezeshkian amesisitiza kwamba, mazungumzo ya nyuklia yasiyo ya moja kwa moja inayofanya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani yako chini uangalizi kamili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei na ametupilia mbali dhana ya kushiriki Iran katika "mazungumzo kwa ajili ya kuzungumza tu."
-
Balozi wa Iran aiasa Kenya kuchukua hatua 'sakata la chai'
Feb 18, 2026 03:53Mwanadiplomasia wa Iran imeiomba serikali ya Kenya kuchukua hatua na kulipatia ufumbuzi sakata la chai la thamani ya Shilingi bilioni 2.6 za nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Iran yamuita balozi wa Ujerumani kulalamikia 'uadui' wa Berlin
Feb 18, 2026 02:54Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imemuita balozi wa Ujerumani hapa mjini Tehran kulalamikia misimamo na hatua za hivi karibuni za uadui zilizochukuliwa na mamlaka za Ujerumani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran: Ulimwengu unawajibika kukabiliana na ukiukaji wa haki za binadamu wa Israel
Feb 17, 2026 03:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa jamii ya kimataifa inawajibika kukabiliana na hatua za utawala wa Israel za kuendelea kukiuka pakubwa sheria katika eneo la Asia Magharibi.
-
Iran: Tumeingia katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Marekani kwa nia njema
Feb 16, 2026 23:05Ismail Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Tehran imeingia katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Marekani kwa mtazamo wenye mwelekeo wa matokeo, huku ikibainisha shaka kuhusu taarifa zinazokinzana za Washington.
-
Sisitizo la Iran la kuendeleza mazungumzo na kubakisha machaguo yake, kuanzia makombora hadi ufungaji wa Lango-bahari la Hormuz
Feb 16, 2026 07:37Wakati mivutano kati ya Iran na Marekani inazidi kuongezeka, Tehran imesisitiza kuwa, machaguo yake yote yako mezani, licha ya mazungumzo yanayoendelea baina yake na Washington.
-
Araqchi: Sarakasi ya Munich dhidi ya Iran imedhihirisha namna Ulaya ilivyopoteza ushawishi wake wa kijiopolitiki
Feb 15, 2026 04:30Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Mkutano wa Usalama wa Munich uliokua na mtazamo dhidi ya Iran umegeuka na kuwa kongamano la sakarakasi na hivyo kudhihirisha namna Ulaya ilivyopoteza ushawishi wake wa kijiopolitiki na umuhimu wa kistratejia.
-
Baqaei: Mashinikizo ya kisiasa hayawezi kudhoofisha haki ya Iran ya kurutubisha urani
Feb 15, 2026 04:28Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa haki "isiyoweza kubatilishwa" ya Iran ya kurutubisha madini ya urani haiwezi kudhoofishwa na mashinikizo ya kisiasa.
-
Kwa nini Grossi amekiri haki ya Iran ya kurutubisha urani?
Feb 13, 2026 07:51Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amekiri kwamba, Iran kama nchi iliyotia saini Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), ina haki ya kurutubisha urani.
-
Kiongozi Muadhamu awashukuru wananchi kwa kuwakatisha tamaa maadui katika maandamano ya mamilioni ya watu
Feb 13, 2026 03:51Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amewasifu na kuwapongeza wananchi wa Iran kwa kujitokeza kwa wingi kote nchini katika maandamano ya maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kusema kuwa maandamano hayo yamewakatisha tamaa maadui.