-
Waziri wa Mambo ya Nje asisitizia tena azma ya Iran ya kutetea haki zake za kisheria za nyuklia
Dec 17, 2025 03:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Sayyid Abbas Araghchi amesisitizia azma ya Jamhuri ya Kiislamu ya kutetea haki zake za kisheria za nyuklia kulingana na Mkataba wa Kuzuia Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), akisema sera za nyuklia za Tehran zingali zinaendana na mfumo wa sheria za kimataifa.
-
Iran yaitaka dunia izuie kuendelea mauaji ya Wapalestina Gaza
Dec 16, 2025 03:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amelaani vikali kuendelea kwa mauaji ya halaiki ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, akiashiria mashambulizi ya mabomu yanayoendelea kufanywa na Wazayuni na kuzuiwa kwa misaada ya kibinadamu.
-
Mauzo ya chai ya Iran nje ya nchi yaongezeka kwa 48%
Dec 16, 2025 03:12Mkuu wa Shirika la Chai la Iran, Habib Jahansaz amesema mauzo ya chai ya Jamhuri ya Kiislamu nje ya nchi katika miezi minane ya kwanza ya mwaka huu wa kalenda ya Iran (ulioanza Machi 21) yameongezeka kwa asilimia 48, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.
-
Iran: Madai ya kumiliki visiwa vya Ghuba ya Uajemi ni dhidi ya mamlaka ya kujitawala na ujirani mwema
Dec 15, 2025 23:58Iran imesema kuwa madai yoyote ya kumiliki visiwa vitatu vya Ghuba ya Uajemi yaani Tomb Kubwa, TombNdogo na Bu Musa ni ukiukaji wa kanuni za ujirani mwema na kutoheshimu mamla ya kujitawala ya nchi nyingine.
-
Iran: IAEA haina haki ya kutaka kukagua vituo vilivyoshambuliwa
Dec 15, 2025 08:05Mkuu wa shirika la nyuklia la Iran amekosoa wito wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA wa kufanya ukaguzi mpya kwenye maeneo ya nyuklia yaliyoshambuliwa, akisisitiza kwamba taasisi hiyo ya UN haina itifaki zilizo wazi za kukagua maeneo ambayo yalishambuliwa na utawala wa Israel na Marekani.
-
Pezeshkian: BRICS inatoa fursa ya ushirikiano imara zaidi wa wanachama
Dec 13, 2025 23:23Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameashiria nafasi na uwezo wa kundi la BRICS na kulieleza kama jukwaa muhimu la kuimarisha maingiliano na uhusiano wa kiuchumi na kisiasa miongoni mwa nchi wanachama.
-
Iran yalaani mwenendo wa madola makubwa wa kuitunukia Israel 'haki maalumu' ya kufanyia uchokozi
Dec 12, 2025 07:33Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, sera za mataifa makubwa katika Asia Magharibi zimetengeneza "haki maalumu kwa ajili ya utawala wa Kizayuni," hali ambayo imeiwezesha Israel kufanya uchokozi wa kijeshi katika eneo zima, ikiwa ni pamoja na dhidi ya Iran, bila kukabiliwa na mjibizo wa maana kimataifa kwa uchokozi wake huo.
-
Iran yakosoa kupunguzwa misaada ya kimataifa kwa wakimbizi wa Afghanistan
Dec 11, 2025 23:08Iran imeikosoa jamii ya kimataifa kwa kushindwa kutimiza hata ahadi za kimsingi za kuwasaidia mamilioni ya wakimbizi wa Kiaghani; ikisema kuwa kupunguzwa misaada kumeifanya nchi hiyo kubeba mzigo mkubwa wa kifedha licha ya indhari za miaka mingi.
-
Mtazamo wa Iran kuhusu vitendo vya Marekani dhidi ya Venezuela: Uzushi hatari unaotishia amani na usalama wa dunia
Dec 11, 2025 05:15Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amevitaja vitendo vya Marekani dhidi ya Venezuela kuwa ni uzushi hatari unaotishia amani na usalama wa dunia.
-
Hatua mpya katika uhusiano wa Iran na Kenya; kianzio katika diplomasia ya Kiafrika ya Tehran?
Dec 09, 2025 09:12Balozi wa Iran nchini Kenya amesema kuwa uhusiano kati ya Tehran na Nairobi umeingia katika hatua mpya.