-
Eran Etzion: Endapo Israel itaingia vitani na Iran, miundombinu yake yote itasambaratishwa
Jul 09, 2018 21:55Naibu Mkuu wa zamani wa Baraza la Usalama wa Taifa la utawala wa Kizayuni wa Israel amesema kuwa, utawala huo huna nguvu ya kuishinda Iran na kwamba, kama utaingia vitani na Iran basi utapata hasara kubwa kwani miundombinu yake itaharibiwa vibaya.
-
India: Tunanunua mafuta ya Iran kwa maslahi yetu ya kitaifa sio ya Marekani
Jul 09, 2018 09:08Waziri wa Mafuta wa India sambamba na kuelezea umuhimu wa kuendelea kununua mafuta ya Iran licha ya tishio la vikwazo vya Marekani, amesema kuwa ununuzi wa mafuta hayo unatokana na maslahi ya kitaifa ya India na sio ya Marekani.
-
Madaktari Wairani washiriki kumbukumbu ya mauaji ya kimbari Srebrenica
Jul 08, 2018 23:23Kundi la madaktari na wasomi wa Iran linashiriki katika kumbukumbu ya 22 ya mauaji ya kimbari yaliyofanywa na Waserbia dhidi ya maelfu ya Waislamu wa Srebrenica huko Bosnia Herzegovina.
-
Iran: Washauri wetu wa kijeshi kusalia Syria kuzima chokochoko za Israel
Jul 08, 2018 09:41Mshauri wa Masuala ya Kimataifa wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, washauri wa kijeshi wa Iran watasalia nchini Syria kuisaidia nchi hiyo ya Kiarabu kuzima chokochoko za mabaki ya magenge ya kigaidi yanayoungwa mkono na nchi ajinabi.
-
Iran yawakamata magaidi 32 wa ISIS wakiwa wanapanga njama
Jul 08, 2018 08:17Mwendesha Mashtaka wa Tehran amesema magaidi wasiopungua 32 wa kundi la kigaidi la ISIS au Daesh wamekamatwa nchini Iran hivi karibuni.
-
Iran yamlaani Trump kwa amri yake yenye kuitusi OPEC
Jul 07, 2018 09:04Iran imesema Rais Donald Trump wa Marekani ameitusi Jumuiya ya Nchi Zinazouza Mafuta ya Petroli kwa Wingi Duniani OPEC, kwa kuiamuru iongeze uzalishaji na ipunguze bei.
-
Iran yasema uwezo wake wa makombora ni kwa ajili ya kujilinda
Jul 07, 2018 03:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa hatua ya Iran ya kuimarisha uwezo wake wa makombora ni kwa ajili ya kujihami.
-
Iran kuwanyonga magaidi 8 wa ISIS waliohusika na hujuma za kigaidi mjini Tehran
Jul 06, 2018 22:09Mahakama nchini Iran imepitisha hukumu ya kuwanyonga magaidi wanane wa kundi la kigaidi la Daesh ambao walihusika katika hujuma dhidi ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, na Haram Takatifu ya Muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Imam Khomeini MA, mwaka 2017 mjini Tehran.
-
Kifurushi 'cha kukatisha tamaa' cha Ulaya; kuendelea JCPOA kutategemea kikao cha Vienna
Jul 06, 2018 09:24Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumza kwa njia ya simu na Angela Merkel, Kansela wa Ujerumani na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa na kuwafahamisha kwamba kifurushi cha kiuchumi cha Umoja wa Ulaya kilichowasilishwa kwa Iran ni cha 'kukatisha tamaa'.
-
Lavrov: Matatizo ya Mashariki ya Kati yatatatuliwa kwa kuishirikisha Iran
Jul 04, 2018 22:09Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia amesisitiza kuwa, kuitaka Iran ipunguze ushawishi wake nchini Syria na Mashariki ya Kati ni kutazama mambo bila ya kuzingatia uhalisia wake.