-
Wananchi wa Iran waandamana kumuunga mkono Sheikh Issa Qassim
May 26, 2017 09:22Wananchi wa Iran leo wameandamana katika mikoa mbalimbali baada ya Swala ya Ijumaa na kutangaza himaya yao kwa Sheikh Issa Qassim mwanazuoni wa Bahrain anayekabiliwa na vitendo vya ukandamizaji vinavyofanywa na vyombo vya usalama vya nchi hiyo.
-
Iran imejenga kiwanda cha tatu cha makombora chini ya ardhi
May 26, 2017 03:24Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imejenga kiwanda cha tatu cha chini ya ardhi cha kuzalisha makombora ya kujihami.
-
Iran yatuma wajumbe wa Quráni katika nchi mbalimbali duniani
May 25, 2017 23:29Kama ilivyo ada yake ya kila mwezi mtukufu wa Ramadhani, mwaka huu pia, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itatuma ujumbe mbalimbali wa Quráni katika nchi tofauti za dunia.
-
Maadhimisho ya Siku ya Afrika yafanyika katika Chuo Kikuu cha Tehran
May 25, 2017 23:27Maadhimisho ya Siku ya Afrika yaliyohudhuriwa na mabalozi wa nchi za Afrika waliopo hapa mjini Tehran pamoja na wanachuo na wapenzi wa masuala ya Afrika, yalifanyika jana Alkhamisi katika Chuio Kikuu cha Tehran.
-
Zarif: Wananchi wa Iran hawaogopeshwi na vitisho
May 25, 2017 23:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema, taifa la Iran ni taifa imara na la watu wasiotetereka hivyo haliogopeshwi na vitisho vyovyote vya Marekani.
-
Iran iko tayari kushirikiana na Sierra Leone katika kupambana na ugaidi
May 25, 2017 03:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria mashambulio ya kigaidi katika baadhi ya nchi za Ulaya na Afrika na kutangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kushirikiana na Sierra Leone katika kupambana na ugaidi na misimamo ya kufurutu mpaka.
-
Kofi Annan amtaka Trump aache misimamo ya chuki dhidi ya Iran
May 24, 2017 03:05Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa Rais wa Marekani Donald Trump kufanya mazungumzo na Iran badala ya kushikilia misimamo yake ya uhasama dhidi ya Tehran.
-
Iran: Mauaji ya waandamanaji Bahrain, matokeo ya awali ya safari ya Trump Riyadh
May 23, 2017 23:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kushambuliwa na kuuawa wananchi wa Bahrain waliokuwa wakishiriki maandamano ya amani ni matokeo ya kwanza ya safari ya hivi karibuni ya Rais wa Marekani, Donald Trump nchini Saudi Arabia.
-
Hizbullah: Iran ni nembo ya izza na uhuru
May 23, 2017 21:50Naibu Katibu Mkuu wa Hibzullah ya Lebanon amesema, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni nembo ya izza na ukombozi duniani.
-
Shamkhani: Baadhi ya nchi zimeligeuza eneo la Mashariki ya Kati ghala la silaha za Magharibi
May 23, 2017 11:25Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema, baadhi ya nchi za eneo zinazofadhili na kuunga mkono ugaidi zinatumia mapato yao ya mafuta kuigeuza Mashariki ya Kati ghala la silaha za Magharibi na kushamirisha machafuko na vitendo vya ukatili.