-
Iran, Russia na Syria zazungumzia mashambulizi ya US dhidi ya Damascus
Apr 12, 2017 03:15Mawaziri wa ulinzi wa Iran, Russia na Syria wamefanya mazungumzo ya simu kuhusu mashambulizi ya makombora ya Marekani dhidi ya kituo cha kijeshi cha Syria, huku pande tatu hizo zikisisitizia umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wao katika vita dhidi ya ugaidi.
-
Kundi la G7 lapokea vizuri juhudi za Iran za kutafuta suluhisho la kisiasa la migogoro
Apr 11, 2017 23:25Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi saba za viwanda duniani maarufu kwa jina la kundi la G7 wamepokea vizuri juhudi za Iran za kuitafutia utatuzi wa kisiasa migogoro wa Mashariki ya Kati
-
Zarif: Uchunguzi wa kimataifa ufanyike kuhusu mashambulizi ya silaha za kemikali Khan Sheikhoun
Apr 11, 2017 23:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametilia mkazo udharura wa kuundwa tume ya kimataifa ya kufanyika uchunguzi kuhusu mashambulizi ya silaha za kemikali yaliyolenga eneo la Khan Sheikhoun nchini Syria.
-
Rouhani: Ushiriki mkubwa katika uchaguzi wa Iran utatuma ujumbe wa umoja na izza kwa ulimwengu
Apr 11, 2017 12:07Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema ushiriki mkubwa wa wananchi katika uchaguzi mkuu unaotazamiwa kufanyika mwezi ujao utawadhihirishia walimwengu namna Jamhuri ya Kiislamu ni taifa lenye izza, umoja na mshikamano.
-
Iran haina wasi wasi kuhusu ibada ya Hija mwaka huu
Apr 11, 2017 03:13Mwakilishi wa Faqihi Mtawala katika masuala ya Hija amesema, kufuatia mapatano yaliyotiwa saini baina ya Iran na Saudi Arabia, hakuna wasi wasi katika utekelezwaji ibada ya Hija mwaka huu kwa mahujaji wa Iran.
-
Iran kuandaa uchaguzi wa amani na wenye ushiriki mkubwa wa wananchi
Apr 11, 2017 03:12Waziri wa Mambo ya Ndani ya Iran amesema uchaguzi ujao wa rais na mabaraza ya Kiislamu ya miji na vijiji utakuwa wa amani, salama, wa kisheria na wenye ushiriki mkubwa wa wananchi.
-
Wagombea urais Iran kuanza kujiandikisha leo
Apr 10, 2017 23:18Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Iran amesema kuwa, wagombea wa duru ya 12 ya urais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wataanza kujiandikisha rasmi leo Jumanne.
-
Rais Rouhani: Shambulio la Marekani Syria lilikuwa kwa ajili ya kufidia kushindwa kwa magaidi
Apr 10, 2017 10:27Rais Hassan Rouhani amelaani shambulio la makombora lililofanywa na Marekani nchini Syria na kueleza kuwa: Shambulio hilo limefanywa kufidia kushindwa kwa magaidi nchini Syria na limewahamasisha magaidi hao kuendelea kufanya jinai zao nchini humo.
-
Iran na Oman zaanza maneva ya uokoaji katika lango la Hormuz
Apr 10, 2017 09:11Vikosi vya majini vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Oman vimeanza maneva ya pamoja ya utafutaji na uokoaji katika maeneo ya mashariki ya Lango la Hormuz na katika maeneo ya kaskazini mwa Bahari ya Hindi.
-
Ulimwengu wa Spoti, Apr 10
Apr 10, 2017 03:35Ufuatao ni mkusanyiko wa matukio muhimu ya spoti ndani ya siku saba zilizopita, kiaifa na kimataifa......