-
Sanders: Inasikitisha kuona Netanyahu anaalikwa kuhutubia Kongresi ya US
Jun 02, 2024 06:58Seneta wa jimbo la Vermont nchini Marekani amewakosoa vikali viongozi wa Kongresi ya nchi hiyo kwa kumualika 'mtenda jinai' Waziri Mkuu wa utawala wa Israel, Benjamin Netanyahu kuhutubia kikao cha pamoja cha Baraza la Wawakilishi na Baraza la Seneti la Marekani.
-
Barua ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa wanachuo wa Marekani wanaotetea Palestina
May 31, 2024 03:58Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika barua aliyowaandikia wanachuo wenye utu wanaotetea wananchi wa Palestina katika vyuo vikuu vya Marekani, ameonyesha mshikamano wake na maandamano ya wanachuo hao dhidi ya uzayuni na kuwataja kuwa sehemu ya mrengo wa muqawama.
-
IFRC yataka Israel isitishe mashambulizi katika Ukanda wa Gaza
May 30, 2024 03:38Mtandao mkubwa zaidi wa misaada ya kibinadamu duniani umesisitizia udharura wa kusitishwa vita katika Ukanda wa Gaza, eneo ambalo mamilioni ya Wapalestina wanakabiliwa na baa la njaa.
-
Brazil yamrejesha nyumbani balozi wake wa Israel kulalamikia jinai za Gaza
May 30, 2024 03:35Brazil imemrejesha nyumbani balozi wake wa Israel kulalamikia mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza, ambayo yamepelekea Wapalestina zaidi ya 36,100 kuuawa shahidi tangu Oktoba, 2023.
-
Licha ya mauaji ya Rafah, US yasema Israel bado haijavuka 'mstari mwekundu' wa Biden
May 29, 2024 03:13Msemaji wa Baraza la Usalama wa Taifa la Marekani John Kirby amedai kuwa Israel haijakiuka "mstari mwekundu" wa Rais Joe Biden wa kuifanya Washington isitishe katika siku za usoni kuipatia Tel Aviv silaha za mashambulizi kwa sababu inavyohisi Marekani Israel haitaanzisha operesheni ya ardhini ya kuuvamia kikamilifu mji wa Rafah wa kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Licha ya amri ya ICJ Israel yaongeza brigedi nyingine ya kijeshi, mbali na 5 zilizoko Rafah
May 29, 2024 03:12Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limetangaza kuwa linatuma kikosi kingine cha mapigano huko Rafah, kusini mwa Ukanda wa Ghaza, kujiunga na brigedi tano ambazo tayari ziko katika mji huo, huku jeshi hilo likipanua wigo wa uvamizi wake katika mji huo.
-
"Vitisho vya nyuklia vya Israel vitabadilisha mlingano wa usalama katika eneo"
May 26, 2024 22:50Katibu wa Baraza la Kistratajia la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesema vitisho vinavyotolewa na maafisa wa utawala wa Kizayuni wa Israel vya kutumia silaha za nyuklia huenda vikawalazimisha wengine kuangalia upya sera zao za nyuklia katika eneo la Asia Magharibi.
-
Uamuzi wa Mahakama ya Hague kuhusu Rafah: Kushindwa kwingine kwa utawala wa Kizayuni
May 26, 2024 22:49Mahakama ya Kimataifa ya Haki iliyo na makao makuu yake mjini The Hague, Uholanzi , ambacho ni chombo cha juu zaidi cha mahakama cha Umoja wa Mataifa, iliamua Ijumaa, Mei 24, kwamba Israel lazima isimamishe "mara moja" mashambulizi yake ya kijeshi huko Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Euro-Med HRM: Hukumu ya Mahakama ya ICJ ni ithibati kwamba Israel imeshavuka mipaka yote
May 26, 2024 01:09Maha Hussaini, Mkurugenzi wa Mkakati wa Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Med Human Rights Monitor, amesema uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ wa kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel usimamishe mara moja mashambulio yake ya kijeshi katika mji wa Rafah ulioko kusini mwa Ukanda wa Ghaza ni hatua muhimu na yenye uzito mkubwa ambayo dunia imekuwa ikiingoja kwa miongo kadhaa, na wala si tangu tu yalipoanza "mauaji ya kimbari" mnamo Oktoba 7.
-
Borrell: Umoja wa Ulaya uchague ama vita au Israel
May 25, 2024 07:33Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amesema EU inapasa kuweka bayana msimamo wake kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) wa kuutaka utawala wa Israel usitishe mara moja mashambulizi yake ya kijeshi mjini Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.