-
Rais wa Kongo DR na mtangulizi wake waafikiana kuhusu mgao wa nyadhifa za baraza la mawaziri
Jul 27, 2019 09:30Waitifaki wa Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wa mtangulizi wake Joseph Kabila wamesema wamefikia makubaliano kuhusu mgao wa nafasi za wizara baina ya kambi hizo mbili za kisiasa.
-
Watu 12 wauawa katika mashambulio ya wanamgambo wa ADF huko DRC
Jul 23, 2019 10:00Watu 12 wameuawa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakiwemo watoto wawili kufuatia mashambulio ya wanamgambo wa kundi la kigaidi la ADF la Uganda.
-
WHO yatangaza Ebola kuwa 'dharura ya kiafya duniani'
Jul 18, 2019 22:04Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuwa ni ''dharura ya kiafya inayohitaji jumuia ya kimataifa kuitazama''.
-
WHO: Yumkini ugonjwa hatari wa Ebola umesambaa hadi nchini Rwanda
Jul 18, 2019 07:31Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mwanamke raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aliyeaga dunia mapema mwezi huu kutokana na homa hatari ya Ebola aliingia nchini Rwanda akiwa ameathiriwa na ugonjwa huo na huenda alisambaza virusi hivyo nchini humo kabla ya kuelekea nchini Uganda alikofia.
-
WHO yatahadharisha kuhusu hatari ya kuenea homa ya Ebola huko Kongo DR
Jul 17, 2019 07:58Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha kuwa mlipuko wa homa ya Ebola ulioukumba mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huwenda ukawa na athari mbaya sana.
-
UN: Kunahitajika mamilioni ya dola kwa ajili ya kupambana na Ebola, DRC
Jul 15, 2019 07:02Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mlipuko wa ugonjwa wa Ebola huko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huwenda ukaendelea kuwepo kwa kipindi kirefu, kuua idadi zaidi ya watu na kugharibu fedha nyingi iwapo nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa hazitatoa mamia ya mamilioni ya dola kwa sasa kwa ajili ya kupambana na kasi ya ugonjwa huo.
-
Mikakati ya Rais Felix Tchisekedi DRC yaanza kuzaa matunda + Sauti
Jul 13, 2019 11:15Mikakati ya Rais Felix Tchisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya kujaribu kuvunja nguvu mirengo ya kisiasa nchini humo inaonekana imeanza kuzaa matunda. Mossi Mwasi na maelezo zaidi…
-
ICC kutoa hukumu dhidi ya 'Terminator' Ntaganda wa DRC leo
Jul 08, 2019 03:11Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) inatazamiwa kutoa hukumu dhidi ya kiongozi wa zamani wa waasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bosco Ntaganda, ambaye anaandamwa na mashitaka 13 ya jinai za kivita na matano ya uhalifu dhidi ya binadamu katika eneo la Ituri, mashariki mwa DRC.
-
WFP: Mamilioni ya Wakongomani wanakabiliwa na uhaba wa chakula
Jul 03, 2019 02:59Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema mamilioni ya wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanahitajia msaada wa dharura wa chakula katika kipindi cha miezi sita ijayo.
-
Jumapili, tarehe 30 Juni, 2019
Jun 29, 2019 23:48Leo ni Jumapili tarehe 26 Mfunguo Mosi Shawwal 1440 Hijria, sawa na tarehe 30 Juni 2019 Miladia.