-
Takriban watu 11 wameuawa na 65 kujeruhiwa katika milipuko 2 kwenye maandamano ya M23 huko Bukavu
Feb 28, 2025 07:34Mabomu mawili yalilipuka siku ya jana Alhamisi kwenye maandamano ya waasi wa M23 huko Bukavu, mji uliotekwa na makundi yenye silaha mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na kuua takriban watu 11 na kujeruhi 65.
-
Mgogoro mashariki mwa DRC waathiri zaidi ya wanafunzi milioni 1
Feb 27, 2025 11:02Kuongezeka kwa mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo waasi wa M23 wameshadidisha mashambulizi dhidi ya vikosi vya serikali, kumesababisha shule 2,594 kufungwa.
-
Hujuma za waasi mashariki mwa Kongo zimeuwa watu 7,000 mwaka huu
Feb 25, 2025 02:30Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa watu zaidi ya elfu saba wameuawa mwaka huu wakati waasi wa kundi la M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wakiteka miji kadhaa katika eneo lenye utajiri wa madini mashariki mwa Kongo.
-
Rais Tshisekedi anapanga kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
Feb 24, 2025 03:04Rais wa Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo anatazamiwa kuzindua serikali ya umoja wa kitaifa ya nchi hiyo. Tina Salama, msemaji wa Ofisi ya Rais wa Kongo amesema, Rais Tshisekedi ataunda serikali ya umoja wa kitaifa na kufanya mabadiliko ya uongozi katika muungano tawala wa nchi hiyo.
-
Mzozo wa DRC: Bunge la Rwanda lalaani azimio la EU dhidi yake
Feb 22, 2025 11:58Bunge la Rwanda limekosoa vikali azimio lililopasishwa hivi karibuni na Bunge la Ulaya, likidai kuwa Rwanda linahusika na mzozo na machafuko yanayoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Waasi wa M23 waingia Bukavu baada ya kutwaa uwanja wa ndege
Feb 15, 2025 07:12Waasi wa M23 wametangaza habari ya kuingia katika jiji la Bukavu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Ugonjwa 'usiojulikana' waua makumi ya watu DRC; mapigano yanaendelea
Feb 14, 2025 12:10Ugonjwa usiojulikana umeua watu zaidi ya 50 katika eneo la Bansakusu, jimbo la Equateur, magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
UN: Maelfu ya raia Kongo wahama makazi yao baada ya M23 kutoa muhula wa masaa 72
Feb 12, 2025 09:20Waasi wa M23 wanaodhibiti miji ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamefunga kwa nguvu kambi za makazi za raia na kuwalazimisha zaidi ya watu 110,000 kuhama makazi yao katika siku za hivi karibuni. Haya yameelezwa na Umoja wa Mataifa.
-
Bunge la Afrika Mashariki lasimamisha vikao vyake kwa muda usiojulikana kwa sababu za kifedha
Feb 10, 2025 07:00Bunge la nchi za Afrika Mashariki, EALA limetangaza kuwa limesimamisha vikao vyake kwa muda usiojulikana kutokana na changamoto za kifedha, zilizosababishwa na baadhi ya nchi wanachama kushindwa kulipa michango yao ya fedha.
-
Jumuiya za SADC na EAC zataka kusitishwa mapigano Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Feb 09, 2025 03:25Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na ile ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC wametoa mwito wa kusitishwa mara moja mapigano mashariki mwa Jamhuuri ya Kidemokkrasia ya Congo.