Pars Today
Askari wanane wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO) wamekamatwa na kuzuiliwa kwa tuhuma za kuhusika na ubakaji na udhalilishaji wa kingono.
Millionea na mwanasiasa wa upinzani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Moise Katumbi amewasilisha jina lake kwa ajili ya kugombea urais nchini humo.
Kanali Mike Mikombe, kamanda wa zamani wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amehukumiwa kifo kutokana na nafasi yake kwenye mauaji ya makumi ya raia waliokuwa wakiandamana dhidi ya vikosi vya Umoja wa Mataifa.
Kiongozi mwandamizi wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Martin Fayulu, alithibitisha jana Jumamosi mjini Kinshasa kwamba atagombea katika uchaguzi wa rais wa Desemba 20.
Mtu mmoja ameuawa wakati gurunedi aina ya RPG lilipoangukia kimakosa katika uwanja wa michezo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani uamuzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuhamisha ubalozi wake kutoka Tel Aviv hadi Quds inayokaliwa kwa mabavu (Jerusalem) na kutaka kuangaliwa upya uamuzi huo.
Wakimbizi wa ndani zaidi ya 60 wakiwemo watoto wadogo 33 wamepoteza maisha kutokana na njaa katika mkoa wa Kwilu, katikati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Waziri wa utawala wa Kizayuni wa Israel amesema Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo karibuni itauhamishia ubalozi wake mjini Quds (Jerusalem) kutoka Tel Aviv.
Jumuiya ya Afrika Mashariki imekiongeza muda wa kuhudumu kikosi cha kikanda cha jumuiya hiyo (EACRF), chenye jukumu la kukomesha mapigano na kuzima uasi huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limelikosoa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kuua makumi ya raia waliokuwa wakiandamana dhidi ya vikosi vya Umoja wa Mataifa.