-
Maafisa wa SADC na EAC watilia mkazo kusitishwa mapigano mashariki mwa Kongo
Feb 08, 2025 07:49Maafisa wa ngazi ya juu kutoka mataifa ya Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika jana walitilia mkazo kusitishwa mara moja mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuzitaka pande zote husika kutoa kipaumbele kwa suala la kufanya mazungumzo ili kuupatia ufumbuzi mgogoro uliopo.
-
UN: Hali ya kibinadamu huko Goma bado ni mbaya licha ya kusimamishwa mapigano
Feb 07, 2025 02:39Hospitali katika mji mkubwa wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Goma, zinatatizika kutibu mamia ya wagonjwa waliojeruhiwa, huku baadhi wakiripoti uhaba wa dawa siku chache baada ya kundi la waasi la M23 kutangaza kusitisha mapigano kwa upande mmoja.
-
Mahakama ya Kijeshi ya DRC yatoa hati ya kukamatwa Corneille Nangaa
Feb 06, 2025 11:17Mahakama ya Kijeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imetoa hati ya kukamatwa kwa Corneille Nangaa, mkuu wa makundi ya waasi wa mashariki mwa nchi hiyo, ikimtuhumu kwa kushindwa kuzuia vitendo vya utesaji chini ya mamlaka yake.
-
Uganda yatuma askari 1,000 zaidi mashariki mwa DRC
Feb 05, 2025 02:40Uganda imeripotiwa kutuma wanajeshi zaidi ya 1,000 wa ziada huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ndani ya wiki moja iliyopita, karibu na eneo ambalo wanajeshi wa serikali ya Kinshasa wanapambana na waasi wa M23.
-
Muungano wa waasi wa mashariki mwa Kongo likiwemo kundi la M23 watangaza kusitisha mapigano
Feb 04, 2025 07:30Muungano kwa jina la The Alliance Fleuve Congo; muungano wa waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unaolijumuisha pia kundi la waasi wa M23 umetangaza kusitisha mapigano kuanzia leo Jumanne Februari 4.
-
Utulivu wa kulegalega washuhudiwa Goma; Mapigano yapungua mashariki mwa DRC
Feb 02, 2025 07:45Ripoti mbalimbali zinaeleza kuwa licha ya kurejea utulivu wa kiwango fulani katika mji wa Goma, makao makuu ya jimbo la Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mashirika ya misaada ya kibinadamu yameonya juu ya kushtadi hali ya mambo huku hospitali zikizidiwa na wagonjwa, uhaba wa vifaa muhimu vya tiba ukishuhudiwa na miili ya watu waliouawa ikiendelea kuonekana mitaani.
-
UN: Watu 700 wameuawa DRC ndani ya siku tano
Feb 01, 2025 07:59Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kukomesha ghasia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ambako mapigano kati ya vikosi vya serikali na waasi wa M23 yamesababisha watu zaidi ya 700 kuuawa huku wengine wasiopungua 2,800 wakijeruhiwa katika kipindi cha siku tano.
-
Watu 25 wauawa katika mapigano mashariki mwa DRC; M23 wadai kuidhibiti Goma
Jan 28, 2025 09:09Zaidi ya watu 22 wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa wakati wa mapigano kati ya waasi wa M23 na vikosi vya serikali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Mkuu wa MONUSCO awataka waasi wa M23 kuondoka Kongo
Jan 27, 2025 08:07Mkuu wa kikosi cha wanajeshi wa kulinda amani cha Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO) amewataka waasi wa kundi la M23 kusitisha harakati zao na kuondoka nchini humo.
-
Waasi wa M23 wauteka mji wa kistratajia mashariki mwa DRC
Jan 22, 2025 02:49Waasi wa M23 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuteka mji wa mashariki wa Minova, njia kuu ya usambazaji wa bidhaa huko Goma, makao makuu ya mkoa wa Kivu Kaskazini.