-
10 wauawa, maelfu wahama makazi yao katika shambulio la M23 la kuuteka mji wa mashariki mwa DRC
Mar 07, 2024 12:02Kundi la waasi la M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) linalodaiwa kuwa na uhusiano na nchi jirani ya Rwanda limeuteka mji wa Nyanzale ulioko eneo la mashariki lililokumbwa na mapigano kufuatia mashambulizi yake yaliyosababisha vifo vya watu wasiopungua 10 mbali na kusababisha maelfu ya wengine kuyahama makazi yao.
-
Wakuu wa majeshi ya SADC wakutana Goma kujadili M23
Mar 03, 2024 07:40Majenerali na maafisa waandamizi wa majeshi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wamekutana mjini Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kujadili stratajia ya kuimarisha operesheni dhidi ya waasi wa M23.
-
Ripoti: Wakimbizi DRC wanakabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu
Feb 18, 2024 12:05Maelfu ya watu waliokimbia makazi yao wanaishi katika kambi zisizo salama kiafya mashariki mwa nchi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutokana na mzozo kati ya waasi na jeshi la nchi hiyo.
-
Askari kadhaa wa Afrika Kusini wauawa na kujeruhiwa Kongo DR
Feb 16, 2024 02:47Wanajeshi wawili wa Afrika Kusini wameuawa huku wengine watatu wakijeruhiwa katika shambulizi la bomu lililolenga kambi ya wanajeshi hao mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Makumi wahofiwa kufa maji baada ya boti 2 kugongana Kongo DR
Feb 14, 2024 11:15Makumi ya watu wameripotiwa kupoteza maisha katika ajali mbaya ya boti iliyotokea magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Watu 11 wauawa katika mapigano ya kikabila magharibi ya DRC
Feb 01, 2024 11:11Watu wasiopungua 11 wameuwa baada ya kuibuka mapigano makali ya kikabila katika mkoa wa Mai-Ndombe, magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Kagame: Rwanda haijahusika kivyovyote na mapigano mashariki ya DRC
Jan 24, 2024 03:37Rais wa Rwanda, Paul Kagame amesema nchi hiyo haijahusika kivyovyote na mapigano na ghasia zinazoendelea kushuhudiwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Tshisekedi ameapishwa leo, makumi ya viongozi wa nchi wamehudhuria
Jan 20, 2024 13:48Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Felix Tshisekedi, ameapishwa hii leo Jumamosi kwa muhula wa pili wa miaka mitano baada ya Mahakama ya Katiba kuthibitisha ushindi wake katika uchaguzi mkuu wa mwezi Desemba mwaka jana.
-
Mkuu wa ujasusi wa M23 auawa katika shambulio la ndege zisizo na rubani DRC
Jan 17, 2024 15:20Mkuu wa kitengo cha ujasusi wa kundi la waasi la M23 ameripotiwa kuuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
UN: Walinda amani wote wataondoka Kongo DR mwishoni mwa 2024
Jan 14, 2024 07:40Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambacho kimesaidia katika vita dhidi ya waasi kwa zaidi ya miongo miwili sasa, kitaondoka kikamilifu nchini humo ifikapo mwezi Disemba mwaka huu.