Jun 21, 2023 03:44
Martin Fayulu, kiongozi wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametishia kuwa huenda asishiriki uchaguzi mkuu ujao, huku mvutano wa kisiasa ukiongezeka nchini humo kabla ya uchaguzi wa rais wa Disemba 20, ambapo Rais Felix Tshisekedi anatarajiwa kugombea muhula wa pili.