Apr 27, 2023 10:50
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) inatafakari kuanza kutumia mfumo wa malipo wa kadi ya Mir ya Russia badala za kadi za Kimagharibi za Visa na MasterCard. Hayo yamesemwa na Muhindo Nzangi Butondo Waziri wa Elimu ya Juu na Vyuo Vikuu wa DRC, katika mahojiano na Sputnik.