-
UN: Maelfu wanahitaji msaada wa dharura DRC kutokana na mafuriko
Jan 13, 2024 11:50Umoja wa Mataifa umesema mamia ya maelfu ya watu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanahitaji msaada wa dharura kutokana na athari za mafuriko katika pembe mbali mbali za nchi hiyo.
-
Félix Tshisekedi atangazwa mshindi uchaguzi wa rais Congo DR, wapinzani wapinga matokeo
Jan 01, 2024 03:06Rais Félix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ametangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Disemba 20, 2023 kwa kupata zaidi ya asilimia 73 ya kura.
-
Hali tete DRC; Matokeo ya uchaguzi wa rais kutangazwa leo
Dec 31, 2023 03:06Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (CENI) inatazamiwa kutangaza matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo leo Jumapili, na hali ya taharuki imetanda huku jamii ya kimataifa ikiwa na wasi wasi wa kuibuka machafuko ya baada ya uchaguzi nchini humo.
-
Mvua, maporomoko ya udongo yaua makumi ya watu DRC
Dec 27, 2023 06:43Watu wasiopungua 22 wamefariki dunia kutokana na maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika mji wa Kananga, katikati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Moise Katumbi ataka uchaguzi wa DRC utenguliwe; upinzani waitisha maandamano
Dec 24, 2023 03:25Wagombea watano wa upinzani katika uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo akiwemo Moise Katumbi wametoa mwito wa kufutiliwa mbali uchaguzi huo, wakidai kuwa zoezi hilo la kidemokrasia limekumbwa na wizi wa kura na uchakachuaji wa matokeo.
-
UN inajiandaa kuanza kuwaondoa taratibu wanajeshi wake huko Kongo
Dec 19, 2023 08:03Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo Jumanne linatarajiwa kukubali ombi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo la kuondolewa nchini humo askari wa kulinda amani wa umoja huo (MONUSCO).
-
Kiongozi wa upinzani Congo DR, Katumbi, aahidi 'kuikomboa nchi'
Dec 10, 2023 11:20Wiki mbili kabla ya uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kiongozi wa upinzani Moise Katumbi amepanua zaidi kampeni zake katika jitihada za kushinda cheo cha juu zaidi nchini humo.
-
Rais wa DRC amfananisha Rais Kagame na Adolf Hitler
Dec 10, 2023 03:03Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amemshabihisha mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame na mtawala wa zamani wa Ujerumani ya Manazi, Adolf Hitler.
-
Kikosi cha EAC chaanza kuondoa wanajeshi wake DRC
Dec 03, 2023 10:42Kikosi cha Kikanda cha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACRF) kimeanza kuwaondoa askari wake katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Mshindi wa Tuzo ya Nobel Kongo afanya mkutano wa kampeni za uchaguzi wa rais katika mji alikozaliwa
Nov 26, 2023 06:43Denis Mukwege, daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo jana alifanya mkutano wa kampeni za uchaguzi wa rais katika mji alikozaliwa na kuahidi kukabiliana na ufisadi na kushughulikia migogoro mbalimbali iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa Kongo katika uchaguzi wa rais wa mwezi ujao wa Disemba.