-
Wasiwasi wa UN kuhusu hali ya wakimbizi wa Congo DR
Dec 09, 2017 16:08Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa, watu karibu milioni 2 wamelazimika kuhama makazi yao mwaka huu pekee huko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kuhofia ukatili na mauaji.
-
Guterres: Mauaji dhidi ya askari wa UN huko Kongo ni 'jinai ya kivita'
Dec 09, 2017 03:45Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali mauaji ya wanajeshi wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo MONUSCO, na kuutaja ukatili huo kama jinai ya kivita.
-
Jean-Pierre Lacroix: Mapigano ya kikabila Sudan Kusini yamechochea hali ngumu
Dec 08, 2017 11:01Mkuu wa operesheni za kusimamia amani za Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mapigano ya kikabila katika nchi ya Sudan Kusini yamekuwa na nafasi kubwa katika kuifanya hali ya mambo ya nchi hiyo izidi kuwa mbaya.
-
Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) walaani shambulio la wanamgambo mashariki mwa Kongo
Dec 06, 2017 22:11Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) imelaani shambulio lililofanywa na wanamgambo katika kituo chao kilichopo Masisi mkoani Kivu ya Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Serikali ya Kongo DR yatuhumiwa kutumia waasi wa M23 kukandamiza maandamano ya wananchi
Dec 05, 2017 12:32Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeituhumu serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwa iliwatumia waasi wa kundi la M23 kukandamiza maandamano ya wananchi yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
-
Wakimbizi 12,000 kutoka DRC waingia Zambia, UNHCR haina fedha za kuwashguhulikia
Dec 04, 2017 04:09Zaidi ya wakimbizi 12,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamekimbilia nchi jirani ya Zambia kutafuta hifadhi kutokana na machafuko Kusini Mashariki mwa nchi yao.
-
Maelfu ya familia zakimbia mashariki mwa Congo DR kwa kuhofia usalama wao
Nov 27, 2017 11:34Maelfu ya wakazi wa mkoa wa Kivu Kaskazini huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamekimbia makazi yao kwa kuhofia mashambulizi yanayofanywa na makundi ya wanamgambo katika eneo hilo.
-
Serikali ya Congo DR yapiga marufuku maandamano ya wapinzani
Nov 27, 2017 04:40Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imepiga marufuku maandamano ya kambi ya upinzani yaliyopangwa kufanyika tarehe 30 mwezi huu wa Novemba kumshinikiz Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo aondoke madarakani.
-
Congo DR, Burkina Faso zawaita nyumbani mabalozi wao Libya kupinga biashara ya utumwa
Nov 22, 2017 23:58Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Burkina Faso ziimewaita nyumbani mabalozi wao nchini Libya kupinga biashara ya utumwa na kuuzwa wahajiri wa Kiafrika nchini humo.
-
Waasi wa Mai-Mai washambulia ngome za jeshi mashariki mwa DRC
Nov 21, 2017 10:09Msemaji wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika mkoa wa Kivu Kusini ulioko mashariki mwa nchi hiyo amesema kuwa, waasi wa Mai-Mai wameshambulia ngome za jeshi katika mji wa Kilembwe.