-
Zarif arejea Tehran kutokea Afrika Kusini
Jun 14, 2018 10:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amerejea hapa Tehran leo asubuhi baada ya kumaliza ziara rasmi nchini Afrika Kusini ambako alionana na kufanya mazungumzo na viongozi wa mbalimbali wa nchi hiyo.
-
Rouhani: Iran itajiondoa JCPOA iwapo haitadhaminiwa maslahi yake
Jun 13, 2018 02:45Rais Hassan Rouhani amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itajiondoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA iwapo itahisi haistafidi wala kupata maslahi yoyote kutokana na mapatano hayo ya kimataifa.
-
Larijani: Iran itachukua hatua muafaka kukabiliana na chokochoko za Marekani
Jun 12, 2018 09:38Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, Ali Larijani ameashiria hatua ya Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran maarufu kama JCPOA, na kusema: 'Hatua hii ya Marekani imeathiri kwa kiasi fulani uwekezaji nchini, na ili kukabiliana na hilo, tayari hatua maufaka zimechukuliwa na mazungumzo yanaendelea."
-
Tahadhari kali ya Putin kuhusu athari mbaya za kujiondoa Marekani katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA
Jun 11, 2018 02:27Rais Vladimir Putin wa Russia amekosoa vikali uamuzi wa Marekani wa kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA akisema unatishia usalama na amani ya Mashariki ya Kati.
-
Kujitoa Marekani kwenye JCPOA na kupoteza itibari katika mazungumzo na Korea Kaskazini
Jun 09, 2018 02:40Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema, kuna ulazima wa kuyadumisha makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA na kubainisha kwamba: Wakati makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yanalegalega, mwafaka wenye uwezekano wa kufikiwa kati ya Marekani na Korea Kaskazini nao pia hautokuwa na itibari yoyote.
-
Zarif: Nchi wanachama wa JCPOA zifidie hasara ilizopata Iran bila kutoa masharti yoyote
Jun 08, 2018 00:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Ili makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yaendelee, lazima nchi zilizosalia kwenye makubaliano hayo pamoja na washirika wengine wa kibiashara watoe hakikisho kwamba hasara ilizopata Iran (kutokana na Marekani kujitoa kwenye JCPOA) zinafidiwa bila masharti yoyote kupitia hatua za kitaifa, kieneo na kimataifa.
-
Hatua mpya za Ulaya kulinda makubaliano ya JCPOA
Jun 07, 2018 05:23Sambamba na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutangaza hatua ya kuimarisha shughuli zake za nyuklia katika fremu ya mapatano ya nyuklia na nchi sita kubwa za dunia mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA), nchi za Ulaya zimeongeza mashauriano na juhudi za kuyalinda yasije yakasambaratika.
-
Madola matatu makuu ya Ulaya yaitahadharisha Marekani na matokeo hasi endapo Iran itajitoa kwenye JCPOA
Jun 06, 2018 22:48Mawaziri wa Mambo ya Nje wa na wa Fedha wa Ujerumani, Uingereza na Ufaransa wamewaandikia barua mawaziri wenzao wa Marekani wakieleza wasiwasi walionao juu ya uwezekano wa Iran kujitoa kwenye makubaliano ya nyuklia na matokeo hasi ya hatua hiyo.
-
Hatua shtukizi na za kivitendo za Iran za kuleta mlingano katika JCPOA
Jun 06, 2018 09:23Uamuzi mpya uliotangazwa na Iran wa kustawisha shughuli zake za nyuklia kufuatia agizo lililotolewa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu umeonyesha kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haiwezi kutiwa shemere na kuburuzwa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, bali hatamu za kuamua nini la kufanya ziko mikononi mwake.
-
EU: Hatua ya Iran ya kuimarisha urutubishaji urani haikiuki JCPOA
Jun 06, 2018 03:03Umoja wa Ulaya umesema tathmini yake ya mwanzo inaashiria kuwa mpango wa Iran wa kuimarisha urutubishaji urani hadi kufikia kiwango cha SWU 190,000 haukinzani na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.