-
Jeshi la Venezuela latangaza tena utiifu wake kwa Rais Maduro
Feb 20, 2019 23:25Waziri wa Ulinzi wa Venezuela ametangaza tena utiifu wake na vikosi vya majeshi ya nchi hiyo kwa Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo na kusema kuwa, makamanda na wanajeshi wa nchi hiyo wanafuata na kuutii amri ya Rais Maduro na wataendelea kusimama naye bega kwa bega hadi tone la mwisho la damu yao.
-
Silaha za Marekani na magaidi wa Israel zapatikana Syria
Feb 19, 2019 04:30Askari usalama wa Syria wamenasa idadi kubwa ya silaha za Marekani na Israel zinazomilikiwa na magaidi huko Rif-Dimashq.
-
Buhari: Jeshi litakabiliana vikali na hatua za kukwamisha uchaguzi ulioakhirishwa
Feb 19, 2019 04:23Rais Muhammadu Buhari ametahadharisha kuwa yoyote anayejaribu kuzuia uchaguzi wa rais ulioakhirishwa nchini humo anahatarisha maisha yake. Rais wa Nigeria ameituhumu pia Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo kwa kutofanya kazi kwa mujibu wa sheria.
-
Iran yazindua nyambizi mpya yenye makombora ya cruise
Feb 17, 2019 23:03Rais Hassan Rouhani wa Iran amezindua nyambizi ya kisasa iliyoundwa hapa nchini ambayo ina uwezo wa kusheheni makombora ya cruise.
-
Jeshi la Sudan: Hatutaruhusu nchi isambaratike kutokana na machafuko
Jan 31, 2019 11:25Jeshi la Sudan limesema kuwa halitaruhusu nchi isambaratike kufuatia maandamano ya nchi nzima yanayoendelea sasa huku Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo akitahadharisha juu ya kuwepo njama ya kuchochea hali ya mchafukoge nchini humo.
-
Maelfu ya wanajeshi wa Marekani waelekea katika mpaka wa Mexico
Jan 30, 2019 03:56Naibu Waziri wa Ulinzi wa Marekani amesema kuwa, maelfu ya wanajeshi wa nchi hiyo wameelekea katika mpaka wa Mexico kwa lengo la kile kilichotajwa kuwa ni kurejesha hali ya usalama katika eneo hilo.
-
Admeri Sayyari: Mfumo wa kijeshi wa Iran ni wa kujihami na kutegemea uwezo wa kuzuia hujuma dhidi yake
Jan 27, 2019 04:31Mkuu wa uratibu wa jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, mfumo wa kijeshi wa Iran ni wa kujihami na unaotegemea uwezo wa kuzuia hujuma dhidi yake na akaongezea kwa kusema, zana zote za kijeshi na kiulinzi za vikosi vya ulinzi zinatengezwa humu humu nchini.
-
Israel yakiri kuwapa msaada wa silaha wapinzani wa serikali ya Syria
Jan 16, 2019 00:58Mkuu wa Majeshi ya Utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kuwa utawala huo umekuwa ikiwapa silaha wapinzani wa serikali ya Syria.
-
Zimbabwe yatumia wanajeshi kuzima maandamano, kadhaa wauawa
Jan 15, 2019 11:08Watu wasiopungua watano wameuawa na maafisa usalama huku maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya mafuta kwa asilimia 150 nchini Zimbabwe yakishtadi.
-
Jeshi la Sudan latangaza uungaji mkono kwa al Bashir, vyama vya upinzani vyajiunga na maandamano ya wananchi
Dec 24, 2018 23:29jeshi la Sudan limetangaza uungaji mkono wake kwa kiongozi anayezongwa na matatizo mengi ya kisiasa na kiuchumi wa nchi hiyo baada ya kushadidi maandamano ya wananchi wanaopinga hali mbaya ya uchumi. Waandamanaji hao pia wametoa wito wa kuondolewa madarakani serikali ya sasa ya Khartoum.