Jun 18, 2021 12:31
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema kuwa, shambulio la jana la ndege za utawala wa Kizayuni dhidi ya kambi za muqawama katika Ukanda wa Ghaza ni chokochoko mpya za Israel zilizolenga kunyanyua mori wa wanajeshi wake waliopata kipigo katika mapigano ya hivi karibuni ya siku 12 ya Ukanda wa Ghaza maarufu kwa jina la vita vya "Upanga wa Quds."