-
Hizbullah: Tutaendelea kuweko Syria hadi hatari ya magaidi itakapoondoka
Sep 04, 2017 22:05Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, harakati hiyo ya mapambano ya Kiislamu ambayo iko Syria kwa ombi la serikali ya nchi hiyo, itabakia nchini humo hadi pale hatari ya ugaidi itakapoondoka.
-
Lebanon yakanusha madai ya kuwepo viwanda vya makombora vya Iran nchini humo
Sep 02, 2017 03:01Waziri Mkuu wa Lebanon amekadhibisha madai yaliyotolewa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inatengeneza viwanda vya kuzalisha makombora katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Jeshi la Lebanon lawekwa mpakani baada ya Madaesh kutimuliwa kwenye mpaka wa nchi hiyo na Syria
Aug 29, 2017 22:41Kufuatia kutimuliwa magaidi wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) linalopata uungaji mkono wa Marekani, Israel na Saudia katika mpaka wa pamoja wa Syria na Lebanon, Jumanne ya jana jeshi la Lebanon lilituma askari wake katika miinuko ya Al-Qalamoun walipokuwako magaidi hao wakufurishaji.
-
Magaidi wa Daesh (ISIS) wajisalimisha kwa Hizbullah ya Lebanon
Aug 27, 2017 10:08Wapiganaji wenye silaha wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) wamejisalimisha kwa vikosi vya muqawama baada ya vikosi hivyo kuwakaribia magaidi hao katika eneo la mpaka wa pamoja wa Lebanon na Syria.
-
Sayyid Nasrullah: Mapambano dhidi ya ugaidi yataendelea Lebanon
Aug 24, 2017 23:53Katibu Mkuu wa chama cha Hizbullah cha nchini Lebanon amesema kuwa, mapambano katika milima ya mpakani mwa nchi hiyo na Syria yataendelea hadi yatakapoangamizwa kikamilifu magenge ya kigaidi.
-
Émile Lahoud: Kusimama kidete Lebanon mkabala na Israel kulitimia kwa himaya ya Iran
Aug 23, 2017 22:03Émile Lahoud Rais wa zamani wa Lebanon amesema kuwa, muqawama wa Lebanon uliweza kusimama kidete mbele ya mashambulio ya utawala ghasibu wa Israel kutokana na himaya na uungaji mkono wa Jamhuri ya kiislamu ya Iran.
-
Umoja wa Kiislamu, njia pekee ya kukabiliana na magaidi wakufurishaji na Wazayuni
Aug 23, 2017 09:16Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema njia pekee ya kukabiliana na vitisho viwili vya magaidi wakufurishaji na Wazayuni ni kuwepo umoja na mshikamano miongoni mwa Waislamu duniani.
-
Maulama ya Kisuni na Kishia wataka kuweko vita vya kweli dhidi ya magaidi barani Afrika
Aug 18, 2017 10:35Maulama wa Kisuni na Kishia wa Lebanon wamesisitiza udharura wa kuweko vita vya kweli na vyenye mpangilio dhidi ya magaidi katika nchi za Kiafarika.
-
Rais wa zamani wa Lebanon: Yemen itashinda vita kama vile Iraq na Syria zilivyowashinda magaidi
Aug 17, 2017 23:46Rais wa zamani wa Lebanon Émile Lahoud amesema kuwa, Wayemen wataibuka washindi dhidi ya vibaraka wa Saudi Arabia, kama ambavyo Syria na Iraq zimepata ushindi dhidi ya magaidi na waungaji wao mkono.
-
Larijani apongeza ushindi wa Hizbullah ya Lebanon katika vita vya siku 33
Aug 15, 2017 23:32Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) ametuma ujumbe tofauti kwa Nabih Berri Spika wa Bunge la Lebanon na Sayyid Hassan Nasrullah Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya nchi hiyo kwa mnasaba wa maadhimisho ya ushindi wa Lebanon katika vita vya siku 33.