-
UN: Mazungumzo ya amani Libya yamalizika; Imarati bado yatuma silaha kimagendo
Oct 01, 2020 02:31Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa mazungumzo ya makundi mbalimbali ya Libya ya kutafuta amani ya nchi yao yamemalizika nchini Misri na matokeo ya mazungumzo hayo ni mazuri.
-
Wahajiri 16 wafariki dunia baada ya boti yao kughariki pwani ya Libya
Sep 26, 2020 12:14Watu wasiopungua 16 wamefariki dunia katika Bahari ya Mediterania baada ya boti yao kuzama, huko pwani ya Libya.
-
Uturuki: Ankara itaendelea kuisaidia serikali ya GNA Libya hata baada ya Sarraj kung'atuka
Sep 22, 2020 02:41Uturuki imetangaza kuwa itaendelea kuiunga mkono serikali inayotambuliwa kimataifa ya Libya licha ya Waziri Mkuu Fayez al-Sarraj kutangaza wiki iliyopita kwamba, anapanga kuondoka madarakani mwishoni mwa mwezi ujao.
-
Sisitizo la Umoja wa Mataifa la kutekelezwa vikwazo vya silaha dhidi ya Libya
Sep 18, 2020 02:42Hali ya wasiwasi kuhusu mgogoro wa kisiasa unaoikabili Libya na hali inayolegalega nchini humo ni mambo ambayo yangali yanaendelea kushuhudiwa licha ya kutangazwa usitishaji vita nchini humo. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio na kutaka kutekelezwa vikwazo vya silaha dhidi ya Libya na kuondolewa mamluki wote katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Waziri Mkuu wa GNA Libya kung'atuka madarakani ifikapo mwishoni mwa Oktoba
Sep 17, 2020 13:09Waziri Mkuu wa Serikali ya Muafaka wa Kitaifa ya Libya GNA amesema, atajiuzulu wadhifa wake huo na kukabidhi hatamu za madaraka kwa uongozi mpya utakaochaguliwa kupitia kamati ya mazungumzo ya amani.
-
Katibu Mkuu wa UN kumteuwa mjumbe maalumu katika masuala ya Libya
Sep 17, 2020 03:01Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limemuomba Katibu Mkuu wa umoja huo Antonio Guterres kufanya uteuzi wa Mjumbe Maalumu ili kusuluhisha mzozo unaoendelea nchini Libya na kuongoza jitihada za kurejesha amani katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
UN yataka kutekelezwa vikwazo vya silaha dhidi ya Libya
Sep 16, 2020 07:47Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio la kutekeleza vikwazo vya silaha dhidi ya Libya na kuondoka mamluki wote katika nchi hiyo ya Kiafrika.
-
Kushadidi mgogoro wa Libya; Waziri Mkuu wa Serikali ya mashariki ajiuzulu
Sep 15, 2020 02:33Mgogoro wa ndani nchini Libya umeshadidi mno. Matatizo ya kiuchumi na kuvurugika maisha, kuongezeka ufisadi na kuendelea vita vya ndani kumewafanya mamia ya wananchi wa nchi hiyo katika siku za hivi karibuni kujitokeza katika miji mbalimbali ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika na kuandamana wakitaka kuhitimishwa mizozo ili kutoa fursa ya kuboreshwa hali ya kisiasa na kiuchumi ya nchi hiyo.
-
'Serikali ya Haftar' huko Libya yajiuzulu kufuatia maandamano ya wananchi
Sep 14, 2020 06:05Serikali ya Libya yenye makao makuu yake mashariki mwa nchi na inayoongozwa na Abdullah Al-Thani, imetangaza kujiuzulu kufuatia maandamano ya siku tatu ya wananchi katika miji mikubwa ya mashariki mwa nchi.
-
Kundi la Haftar lakiuka makubaliano ya usitishaji vita Libya
Sep 07, 2020 03:34Jeshi la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya limetangaza kuwa, vikosi vya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na Khalifa Haftar vimekiuka makubaliano ya usitishaji vita.