-
Kubatilisha Khalifa Haftar makubaliano ya Skhirat na kujitangaza kuwa kiongozi wa Libya
Apr 29, 2020 00:48Katika hali ambayo mapigano baina ya vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa Libya na wanamgambo watiifu kwa Khalifa Hatar yangali yanaendelea, jenerali huyo muasi amechukua hatua ya upande mmoja ya kuvunja makubaliano ya kisiasa ya Skhirat na kujitangaza kuwa kiongozi wa nchi hiyo.
-
Wanamgambo watiifu kwa Jenerali muasi Haftar washambulia msikiti katika mji mkuu wa Libya
Apr 27, 2020 07:52Kikosi cha mizinga cha wanamgambo wanaoongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar, kimeshambulia msikiti katika mji mkuu wa Libya, Tripoli pamoja na maeneo ya makazi ya raia kandokando ya mji huo.
-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa Libya yapinga mpango wa EU wa kuzuia kuingizwa silaha nchini humo
Apr 25, 2020 13:13Vita vya ndani nchini Libya vilivyoanza baada ya kung'olewa madarakati dikteta wa zamani wa nchi hiyo, Muammar Gaddafi vimeshika mwelekeo unaotia wasiwasi mkubwa zaidi tangu Aprili mwaka jana 2019 kufuatilia mashambulizi ya wapiganaji wa linalojiita jeshi la taifa la Libya chini ya uongozi wa Khalifa Haftar, lengo likiwa ni kuudhibiti mji mkuu, Tripoli na kuing'oa madarakani Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa.
-
Ripoti: UAE inashirikiana na Sudan kuunga mkono waasi wa Haftar nchini Libya
Apr 25, 2020 11:04Gazeti moja la Libya limefichua kuhusu mapatano mapya ya Sudan na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa lengo la kumuunga mkono kinara wa waasi Libya, Jenerali Khalifa Haftar.
-
Libya: Watawala wa Imarati ndio wanaosababisha maafa nchini mwetu
Apr 23, 2020 11:38Waziri wa Mambo ya Ndani wa Serikali ya Maridhiano ya Kitaifa ya Libya amesema kuwa, watawala wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ndio wanaosababisha maafa nchini Libya kutokana na wanamgambo wake walioko chini ya jenerali muasi Khalifa Haftar kutumia gesi za sumu katika mashambulizi yao.
-
Jeshi la serikali ya Libya ladhibiti ngome kadhaa za kijeshi
Apr 21, 2020 11:38Wanajeshi wa serikali inayoongozwa na Fayez al-Sarraj, sambamba na kusonga mbele kuelekea mji wa Tarhunah na kudhibiti moja ya ngome muhimu za wanamgambo wa Khalifa Haftar, wamedhibiti pia ngome kadhaa eneo hilo.
-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa Libya yaanzisha operesheni ya kukomboa Tarhunah
Apr 19, 2020 02:35Jeshi la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya limeanzisha operesheni kubwa ya kijeshi ya kudhibiti mji wa Tarhunah, ngome kuu iliyiobakia ya askari watiifu wka mbabe wa kivita, jenerali mstaafu Khalifa haftar huko magharibi mwa Libya.
-
Wanamgambo wa Haftar wafanya mashambulio makubwa dhidi ya mji mkuu Tripoli
Apr 18, 2020 07:53Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya imetangaza kuwa, wanamgambo wanaoongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar wamefanya mashambulio makubwa dhidi ya mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Misri, Saudia na UAE zaandaa mkakati mpya kuliokoa kundi la Haftar lisisambaratishwe katika vita vya Libya
Apr 16, 2020 14:39Sambamba na kushindwa mtawalia kundi liitwalo Jeshi la Taifa la Libya (LNA) katika hujuma na mashambulio linayofanya ya kutaka kuudhibiti mji mkuu wa nchi hiyo, Tripoli, Misri, Saudi Arabia na Imarati (UAE) zimefikia makubaliano ya kuwapatia misaada zaidi wapiganaji wa kundi hilo.
-
Mamia ya wafungwa watoroka jela nchini Libya
Apr 16, 2020 07:50Mamia ya wafungwa waliokuwa wamefungwa jela katika mji wa Surman wa magharibi mwa mji mkuu wa Libya, Tripoli, wametoroka jela na kukimbilia kusikojulikana.