-
Seif al Islam Gaddafi akutana na viongozi wa ngazi za juu wa Imarati na Misri
Sep 17, 2018 15:27Baadhi ya duru za ngazi za juu za Libya na Misri zimetangaza kuwa, Seif al Islam, mtoto wa kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi, amekutana na viongozi wawili wakubwa wa Umoja wa Falme za Kiarabu na Misri.
-
Wakazi wa mji mkuu wa Libya, Tripoli walalamikia hali mbaya ya usalama
Sep 17, 2018 04:04Wakazi wa mji mkuu wa Libya, Tripoli jana walifanya maandamano wakilalamikia hali mbaya ya usalama katika mji huo mkuu na kutaka kuboreshwa hali ya maisha nchini humo.
-
Sheria ya kura ya maoni kuhusu katiba ya Libya yapasishwa
Sep 14, 2018 15:27Bunge la Libya lenye makao yake mashariki mwa nchi limefanya kikao cha dharura na kupasisha suala la kufanyika kura ya maoni kuhusu katiba ya nchi hiyo.
-
Mpango wa kundi la amani la Libya wa kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo
Sep 13, 2018 14:13Mkuu wa kundi la amani la Libya amesema kuwa kumependekezwa mpango mpya wa kitaifa kwa ajili ya kurejesha amani nchini humo.
-
Sarraj: Uchaguzi hauwezi kufanyika Libya katika mazingira ya sasa
Sep 12, 2018 14:10Waziri Mkuu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya amesema ni muhali kufanyika uchaguzi nchini humo katika mazingira ya hivi sasa.
-
Uwanja wa ndege wa Tripoli, Libya walengwa kwa kombora
Sep 12, 2018 07:39Duru za habari leo asubuhi zimeripoti kuwa uwanja wa ndege wa Tripoli mji mkuu wa Libya umeshambuliwa kwa kombora.
-
Mamia ya wahajiri wafariki dunia karibu na pwani za Libya
Sep 11, 2018 07:32Zaidi ya wahajiri 100 kutoka nchi za Afrika wamefariki dunia katika kipindi cha siku chache zilizopita baada ya boti zao kuzama katika maji ya bahari ya Mediterania karibu na pwani za Libya.
-
Watu wenye silaha washambulia makao makuu ya Shirika la Mafuta la Libya
Sep 10, 2018 14:41Watu kadhaa waliokuwa na silaha leo Jumatatu wameyashambulia makao makuu ya Shirika la Taifa la Mafuta la Libya (NOC) huko Tripoli mji mkuu wa nchi hiyo. Watu walioshuhudia wamesema kuwa, sauti za milipuko zilisika kabla ya watu waliojeruhiwa kutolewa katika jengo la shirika hilo kwa kutumia magari ya ambulansi.
-
Kamanda wa Jeshi la Libya adai, jeshi la Algeria limeivamia Libya
Sep 09, 2018 16:03Kamanda wa jeshi la taifa la Libya amedai kuwa Algeria imeingiza wanajeshi wake katika ardhi ya nchi hiyo.
-
Makundi hasimu Libya yafikia makubaliano ya kusimamisha vita mjini Tripoli
Sep 05, 2018 02:59Kamati ya Umoja wa Mataifa ya kusimamia masuala ya Libya jana jioni ilitangaza habari ya kufikiwa makubaliano ya kusimamisha vita baina ya makundi yenye silaha mjini Tripoli.