-
Misri na Imarati zapinga kufanyika uchaguzi wa Rais na Bunge nchini Libya
Jun 10, 2018 02:49Misri na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) zimeelezea kutofurahishwa kwao na maamuzi wa mkutano wa mjini Paris Ufaransa kuhusiana na Libya na kusema kuwa zinapinga uchaguzi wa Rais na Bunge uliopangwa kufanyika nchini humo tarehe 10 Disemba mwaka huu.
-
Jeshi la Taifa la Libya ladhibiti asilimia 80 ya mji wa Derna
Jun 09, 2018 16:59Msemaji wa Jeshi la Taifa la Libya amesema kuwa jeshi hilo linadhibiti asilimia 80 ya mji wa Derna.
-
UN yawawekea vikwazo vigogo 6 kwa kuhusika na magendo ya binadamu Libya
Jun 08, 2018 06:53Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza kuwawekea vikwazo vigogo sita wanaotuhumiwa kuhusika na biashara haramu ya magendo ya binadamu nchini Libya.
-
Jeshi la Taifa la Libya ladhibiti asilimia 75 ya mji wa Derna
Jun 05, 2018 14:04Vikosi vinavyojiita Jeshi la Taifa la Libya vinavyoongozwa na Jenerali Khalifa Haftar vimetangaza kuwa vimeshafanikiwa kukomboa asilimia 75 ya mji wa Derna wa mashariki mwa nchi hiyo.
-
UN: Wafanya magendo ya binadamu waua wahajiri 12 Libya
Jun 01, 2018 13:53Umoja wa Mataifa umesema wahajiri 12 wameuawa kwa kupigwa risasi na wafanya magendo ya binadamu, walipokuwa wakijirabu kukimbia kambini nchini Libya.
-
Wahajiri haramu 221 waondolewa nchini Libya
Jun 01, 2018 00:55Idara ya wahajiri na wahamiaji nchini Libya imetangaza habari ya kuondolewa wahajiri haramu 221 nchini humo.
-
Wanane wauawa na kujeruhiwa katika mripuko wa bomu mjini Derna, Libya
May 28, 2018 14:32Watu wanane wameuawa na kujeruhiwa kwenye mripuko wa bomu uliotokea katika mji wa Derna wa mashariki mwa Libya.
-
Pande hasimu katika mgogoro wa Libya kukutana Paris ili kuondoa mkwamo wa kisiasa
May 27, 2018 07:41Pande hasimu nchini Libya zitakutana siku ya Jumanne mjini Paris, Ufaransa kwa madhumuni ya kufikia makubaliano juu ya ramani ya njia ya kisiasa inayolenga kutatua masuala yanayozozaniwa na pande hizo ili kuandaa mazingira ya kufanyika uchaguzi baadaye mwaka huu.
-
Wahajiri zaidi ya 100 watoroka kambi za wafanyamagendo ya binadamu nchini Libya
May 27, 2018 02:34Duru za Libya zimetangaza kuwa wahajiri zaidi ya 100 wametoroka kwenye kambi kadhaa zinazodhibitiwa na wafanyamagendo ya binadamu katika mji wa Bani Walid magharibi mwa nchi hiyo.
-
Wahajiri 1,500 waokolewa katika bahari ya Mediterranean
May 26, 2018 07:53Takriban wahajiri 1,500 wamenusuriwa wakiwa katika safari hatarishi katika bahari ya Mediterranean, kwenye operesheni zilizofanyika siku ya Alkhamisi na jana Ijumaa.