-
Waafrika Kusini wajiunga na wageni katika maandamano ya kulaani 'xenophobia'
Sep 15, 2019 02:50Wananchi wazalendo wa Afrika Kusini wamejiunga na raia wa kigeni wanaoishi na kufanya kazi nchini humo, katika maandamano ya kulaani ghasia na mauaji yanayowalenga raia wa kigeni hususan Waafrika wanaoishi nchini humo.
-
Vinara wa jaribio la mapinduzi Burkina Faso wahukumiwa kifungo cha miaka 20 jela
Sep 02, 2019 22:37Waitifaki wawili wakubwa wa rais aliyeondolewa madarakani nchini Burkina Faso, Blaise Compaore, wamehukumiwa vifungo vya hadi miaka 20 jela kwa kupatikana na hatia ya kupanga mapinduzi ya mwaka 2015 dhidi ya serikali ya mpito nchini humo.
-
Independent: Wanawake wamepuuzwa katika mfumo mpya wa utawala Sudan
Aug 05, 2019 07:42Gazeti la Independent linalochapishwa nchini Uingereza limendika kuwa, mfumo mpya wa utawala nchini Sudan umepuuza nafasi na mchango mkubwa wa wanawake katika mapinduzi yaliyouondoa madarakani utawala wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Omar al Bashir.
-
Waandamanaji wanne wauawa katika mji wa Omdurman nchini Sudan
Aug 02, 2019 03:33Waandamanaji wanne wanaripotiwa kuuawa kwa kupigwa risasi katika maandamano yaliyofanyika jana katika mji wa Omdurman huko nchini Sudan, huku makumi ya wengine wakijeruhiwa.
-
Wazambia waandamana kulalamikia ufisadi wa serikali
Jul 21, 2019 08:07Maelfu ya wananchi wa Zambia wamefanya maandamano kulalamikia ufisadi mkubwa wa kifedhi ndani ya serikali ya nchi hiyo.
-
Wanigeria waendeleza maandamano ya kutaka kuachiwa huru Zakzaky
Jul 20, 2019 02:59Waislamu na wanaharakati nchini Nigeria jana Ijumaa waliendeleza maandamano ya kutaka kuachiwa huru Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo licha ya kukabiliwa kwa mkono wa chuma na maafisa usalama wa nchi hiyo.
-
Jeshi la Nigeria laendelea kumwaga damu za wafuasi wa Zakzaky
Jul 17, 2019 02:52Mtu mmoja ameuawa na maafisa usalama katika mji wa Kano nchini Nigeria wakati wa maandamano makubwa ya kushinikiza kuachiliwa huru Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria anayeshikiliwa korokoroni kwa miaka kadhaa sasa.
-
Maelfu waandamana Marekani kupinga udhalilishaji wa Trump kwa wahajiri
Jul 13, 2019 07:59Maelfu ya watu wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya Marekani, kupinga sera hasi za utawala wa Rais Donald Trump dhidi ya wahajiri wanaozuiliwa katika vituo vya mpaka wa nchi hiyo, na pia dhidi ya mpango wa kuwakamata na kuwatimua nchi humo wahajiri ambao hawajasajiliwa.
-
Pande hasimu za Sudan zakubaliana kugawana madaraka
Jul 04, 2019 22:25Wawakilishi wa Baraza la Kijeshi la Mpito nchini Sudan na muungano wa upinzani wa Uhuru na Mabadiliko wameafikiana juu ya suala la kugawana madaraka katika kipindi cha mpito kuelekea katika uchaguzi.
-
Israel yawatia mbaroni makumi ya Wayahudi wa Kiethiopia, maandamano yashtadi
Jul 04, 2019 21:54Makumi ya Wayahudi wenye asili ya Ethiopia wamekamatwa na jeshi la Polisi la utawala haramu wa Israel huku maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi na ukandamizaji wa polisi wa utawala wa Kizayuni wa Israel yakishtadi.