-
Qalibaf asema enzi ya ndege za Marekani aina ya F-35 “kuwindwa” imeanza
Sep 19, 2026 11:59Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema enzi ambayo ndege za kisasa kabisa za kivita za Marekani aina ya F-35 na F-15 zinafuatiliwa na kulengwa tayari imeanza, wakati ripoti zikionyesha kuongezeka kwa shinikizo na uharibifu kwa jeshi la Marekani, miezi saba baada ya Washington kuanzisha vita haramu dhidi ya Iran.
-
“Machozi ya kinafiki”: Araghchi amjibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa kuhusu madai ya haki za binadamu
Sep 19, 2026 11:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amejibu madai ya hivi karibuni yaliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noël Barrot, aliyeshutumu Iran kwa ukiukaji wa haki za binadamu, huku akiikosoa Paris kwa ukimya wake kuhusu mauaji ya watoto wa shule wa Iran yaliyosababishwa na Marekani.
-
Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa: Marekani imetenda uhalifu wa kivita nchini Iran
Sep 18, 2026 03:54Tume ya Kutafuta Ukweli ya Umoja wa Mataifa imetangaza kwamba, baada ya kufanya uchunguzi na kuchambua ushahidi, imefikia hitimisho kwamba mashambulizi ya Marekani dhidi ya Minab na Lamerd yalikuwa ni uhalifu wa kivita.
-
Trump apanga kuipatia Israel 'shehena kubwa zaidi ya mabomu katika historia ya Marekani'
Sep 16, 2026 03:34Ripoti moja inasema, serikali ya Trump inaandaa mpango wa kuupatia utawala wa kizayuni wa Israel shehena ya mabomu 40,000 yenye uzito wa pauni 2,000 kila moja, ambayo thamani yake ni dola bilioni 2.8.
-
Rais wa Iran aihimiza BRICS kulinda kanuni ya kutotumia mabavu
Sep 13, 2026 11:29Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, ametoa wito kwa kundi la mataifa yanayoinukia kiuchumi la BRICS kuchukua jukumu “lenye ufanisi zaidi” katika kulinda mamlaka ya kitaifa na kusimamia kanuni ya kimataifa ya kutotumia nguvu, hasa katika kipindi hiki cha sasa chenye changamoto nyingi.
-
Hifadhi ya makombora ya Marekani yaathiriwa pakubwa na vita vya Iran
Sep 09, 2026 11:05Vita na Iran vimepunguza pakubwa akiba ya makombora ya Marekani na kuibua vizuizi katika uzalishaji katika sekta ya ulinzi huku Washington ikilazimika Washington kupima uwezo wake wa kuhuisha upya akiba ya makombora ili kuwa tayari kukabiliana na migogoro mingine.
-
Katibu Mkuu wa Harakati ya Nujaba: Kuanzia mwezi ujao, hatutambakisha hai mwanajeshi hata mmoja wa Marekani nchini Iraq
Sep 03, 2026 09:09Katibu Mkuu wa harakati ya al Nujaba ya Iraq amesema kwamba Kambi ya Muqawama imejitayarisha kikamilifu kwa ajili ya kuwafukuza wanajeshi wa kigeni nchini humo tarehe 30 mwezi huu wa Septemba, na kwamba baada ya tarehe hiyo, hatutamwacha hai hata mwanajeshi mmoja wa Marekani atakayesalia nchini Iraq.
-
Viongozi wa Jumuiya ya Shanghai walaani vikali vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
Sep 02, 2026 02:51Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) wamelaani vikali vita vya kichokozi vya Marekani pamoja na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kupitia azimio lao la pamoja, wakionya kwamba jinai na chokochoko hizo zinaweka amani na usalama wa kimataifa katika hatari kubwa mno.
-
IRGC yamuadhibu vikali mchokozi kwa kupiga kambi za Marekani Jordan baada ya kushambulia Kisiwa cha Larak
Aug 31, 2026 04:43Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuwa Kikosi chake cha Anga kimeshambulia maeneo na kambi za kijeshi za Marekani huko Jordan, na kutoa jibu la haraka kwa shambulio la kigaidi la Marekani katika Kisiwa cha Larak nchini Iran jana usiku.
-
Mauzo ya Mafuta ya Iran kwa China yaimarika licha ya vita vya kiuchumi vya Marekani
Aug 30, 2026 03:35Takwimu mpya zinaonyesha kuwa mauzo ya mafuta ya petroli ya Iran kuelekea China yameendelea kuwa imara kwa kiasi kikubwa mwaka huu, licha ya Marekani kushadidisha vita vyake vya kiuchumi na kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, huku Tehran ikithibitisha kuendelea kwa usambazaji wa mafuta ghafi kwa wateja wake wa kimataifa bila kusitishwa.