-
Zarif: Liwe liwalo, Iran itaendelea kuuza mafuta yake nje
Jul 14, 2019 02:07Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria vikwazo haramu vya Marekani dhidi ya taifa hili na kusisitiza kuwa, Tehran itaendelea kuyauza mafuta yake nje ya nchi bila kubabaishwa na chochote.
-
Ujasusi mpya wa serikali ya Marekani dhidi ya raia kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi
Jul 14, 2019 01:30Baada ya mashambulizi ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani Serikali ya Federali ya nchi hiyo ilitunga sheria mpya za kudukua kumpyuta na mitandao ya intaneti ya raia ikisaidiwa na Kongresi kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi. Mwishoni mwa kipindi cha utawala wa Barack Obama zilifanyika jitihada za kupunguza udukuzi na operesheni hizo za ujasusi dhidi ya raia wa Marekani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq: Kujitoa Marekani katika JCPOA, sababu kuu ya mgogoro Mashariki ya Kati
Jul 13, 2019 22:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq amefanya mazungumzo na Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya mjini Baghdad ambapo alisema kuwa hatua ya Marekani ya kujitoa kwa upande mmoja katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni sababu kuu ya mgogoro katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Maelfu waandamana Marekani kupinga udhalilishaji wa Trump kwa wahajiri
Jul 13, 2019 07:59Maelfu ya watu wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya Marekani, kupinga sera hasi za utawala wa Rais Donald Trump dhidi ya wahajiri wanaozuiliwa katika vituo vya mpaka wa nchi hiyo, na pia dhidi ya mpango wa kuwakamata na kuwatimua nchi humo wahajiri ambao hawajasajiliwa.
-
Uturuki yaanza kupokea mfumo wa makombora wa S-400 kutoka Russia
Jul 12, 2019 20:38Uturuki imepokea shehena ya kwanza ya mfumo wa makombora wa S-400 kutoka Russia licha ya makelele na vitisho vya Marekani.
-
China: Marekani isicheze na moto katika kadhia ya Taiwan
Jul 12, 2019 11:08Waziri wa Mambo ya Nje wa China ameionya vikali Marekani isijaribu kucheza na moto kuhusiana na suala la Taiwan, huku akikosoa vikali mpango wa Washington wa kukiuzia silaha kisiwa hicho ambacho Beijing inasisitiza kuwa ni milki yake.
-
Kamanda wa IRGC: Uingereza na Marekani zitajuta kwa kuizuilia meli ya mafuta ya Iran
Jul 11, 2019 21:56Naibu Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) ameonya kuwa, Uingereza na Marekani zitajuta kutokana na hatua ya London ya kusimamisha na kuzuilia meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal Tariq (Gibraltar).
-
Zarif: Wamarekani wametengwa katika siasa za kimataifa
Jul 11, 2019 07:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezitaja siasa na machaguo yasiyofaa ya Marekani kuwa miongoni mwa sababu za ushindi wa muqawama na kutengwa Washington katika uga wa siasa za kimataifa.
-
Aoun: Kuiwekea vikwazo Hizbullah ni kuivunjia heshima Lebanon
Jul 11, 2019 06:52Rais wa Lebanon amesema kuwa vikwazo vya Marekani dhidi ya wawakilishi wa harakati ya Hizbullah ya nchi hiyo ni sawa na kuivunjia heshima Lebanon.
-
Russia: Marekani haina haki ya kuikosoa Iran kuhusiana na JCPOA
Jul 11, 2019 03:48Mwakilishi wa Russia katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia IAEA amesema kuwa Marekani haina haki yoyote ya kisheria ya kuikosoa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na hatua yake ya kupunguza ahadi zake kuhusiana na mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA.