-
Kamanda Mkuu wa US Ulaya: Mauzo ya silaha za Marekani kwa Ulaya yameongezeka kwa 600%
Apr 09, 2025 03:04Kamanda Mkuu wa Marekani katika Kamandi ya jeshi la nchi hiyo barani Ulaya amesema, mauzo ya silaha za Marekani kwa nchi za Ulaya yameongezeka kwa asilimia 600 tangu vilipoanza vita kati ya Russia na Ukraine na akaongeza kuwa, thamani ya kiwango cha silaha zilizoagizwa na nchi za Ulaya tangu vilipoanza vita kati ya Russia na Ukraine hadi sasa imefikia dola bilioni 265.
-
Ndege za kivita za Marekani zashambulia Yemen karibu mara 30 katika muda wa chini ya siku moja
Apr 08, 2025 06:47Marekani imefanya karibu mashambulizi 30 ya anga katika majimbo kadhaa kote nchini Yemen katika muda wa chini ya siku moja, na kushadidisha uchokozi wake dhidi ya taifa hilo, katika kile ambacho wataalamu wamekitaja kuwa ni harakati za kujishinda yenyewe za kusitisha bila mafanikio operesheni za Sana'a zinazotekelezwa dhidi ya Israel na waungaji mkono wake kwa ajilii ya kuwatetea wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
-
China yaapa 'kupambana hadi mwisho' dhidi ya ushuru wa Trump
Apr 08, 2025 06:15Wizara ya Biashara ya China imeionya Marekani dhidi ya kuingia katika msururu wa vikwazo vya kibiashara vya 'kujibishana mapigo' baada ya rais wa nchi hiyo Donald Trump kutishia kuweka ushuru wa ziada kwa bidhaa za China zinazoingizwa nchini Marekani.
-
Mamia ya familia zalazimika kukimbia baada ya RSF kushambulia vijiji Darfur, Sudan
Apr 08, 2025 06:12Mamia ya familia zimefurushwa kutoka vijiji viwili magharibi mwa Sudan baada ya mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF). Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM).
-
Msemaji wa Taliban: Askari wa Marekani hawawezi kuruhusiwa kuwepo ndani ya ardhi ya Afghanistan
Apr 08, 2025 06:11Msemaji wa serikali ya muda ya Afghanistan amesisitiza kuwa haiwezekani askari wa Marekani waruhusiwe kwenda na kuwepo ndani ya ardhi ya nchi hiyo.
-
Araghchi: Iran, US zitafanya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja Oman
Apr 08, 2025 03:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesema Jamhuri ya Kiislamu na Marekani zitafanya "mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya ngazi ya juu" nchini Oman karibuni hivi.
-
Ushuru wa Trump; Masoko ya hisa ya US yazidi kuporomoka
Apr 08, 2025 03:24Hisa za Marekani zimeendelea kuporomoka kwa siku ya tatu mfululizo, huku mashirika na wawekezaji wakishindwa kuelewa malengo ya mipango mipya ya ushuru ya Rais wa nchi hiyo, Donald Trump.
-
Hitilafu za viongozi wa Ulaya kuhusu jibu la vita vya ushuru vya Trump
Apr 07, 2025 23:08Tangazo la kutoza ushuru mpya la Rais wa Marekani, Donald Trump, dhidi ya nchi 180 duniani, zikiwemo nchi za Umoja wa Ulaya, limeibua hisia tofauti kutoka kwa nchi mbalimbali duniani.
-
Maandamano ya kumpinga Trump yamesababishwa na mambo mengi
Apr 07, 2025 22:57Huku wananchi wa Marekani wakiendelea kukasirishwa na siasa za kidikteta na uingiliaji kati za Trump, Elon Musk na serikali yao, wataalamu wanasema kuna sababu nyingi zilizopelekea mamia ya maelfu ya watu wajitokeze kote Marekani na nje ya Marekani kupinga siasa za Washington.
-
Iran: Vitisho vya US vinakinzana na wito wake wa diplomasia
Apr 05, 2025 23:29Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amekosoa lugha ya vitisho dhidi ya Tehran, akisisitiza kuwa nchi hii iko tayari kufanya mazungumzo lakini "katika mazingira ya usawa."