-
Moscow: EU imekiri kuwa inahudumia ubeberu wa Marekani
Mar 26, 2024 22:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema matamshi ya karibuni ya Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ni ungamo la Magharibi kwamba inajihusisha na mgogoro wa Ukraine ili kuisaidia Marekani kudumisha nafasi yake ya ubeberu duniani.
-
Undumakuwili wa Marekani kuhusiana na utawala wa Kizayuni na vita vya Gaza
Mar 25, 2024 22:39Marekani, ikiwa ni mshirika muhimu zaidi na muungaji mkono asiye na masharti wa utawala wa Kizayuni wa Israel, inatekeleza sera ya undumakuwili kuhusu utawala huo na jinai zake. Kwa upande mmoja, katika kitendo cha kuonyesha mshikamano na Israel, Washington imetangaza msaada mpya wa kijeshi kwa utawala huo sambamba na kukata misaada kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Wapalestina UNRWA.
-
Kula mweleka njama za Marekani za kuunga mkono mauaji ya kimbari ya Israel kwenye UN
Mar 23, 2024 08:11Azimio lililopendekezwa na Marekani la kuunga mkono mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ghaza limegonga ukuta baada ya kupigiwa kura ya veto na Russia na China ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Wito wa maseneta 19 wa Marekani wa kuundwa taifa huru la Palestina
Mar 22, 2024 22:59Maseneta 19 wa chama cha Democratic wametoa wito wa kuundwa taifa huru la Palestina katika barua yao iliyotumwa kwa Rais wa Marekani, Joe Biden.
-
Palestina: Safari za Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani katika eneo hazina tija yoyote
Mar 21, 2024 10:37Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imesema diplomasia inayofanywa na Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani Anthony Blinken katika Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) bado haijatoa "matokeo yoyote ya kuonekana" kwa ajili ya Ghaza.
-
Misri: Operesheni ya kijeshi ya Israel huko Rafah itakuwa na matokeo mabaya
Mar 18, 2024 23:08Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri amesema Marekani inapasa kuileza wazi Israel kuhusu taathira hasi na matokeo mabaya ya utawala wa Kizayuni kuushambulia kijeshi mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Joe Biden akiri kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu Marekani
Mar 17, 2024 23:03Ijumaa, Februari 15, Rais Joe Biden wa Marekani huku akikiri kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu nchini humo tangu kuanza mashambulizi ya Wazayuni huko Gaza alisema: 'Waislamu kote duniani wanapitia hali ngumu kutokana na imani yao.'
-
Jihadul Islami: US na Isreal zinafuatilia malengo sawa Gaza
Mar 16, 2024 03:50Afisa wa ngazi ya juu wa Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina amesema pamoja na unafiki na hadaa za Marekani, lakini dola hilo la kiistikbari linafuatilia malengo yanayoshabihiana na ya Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Jaribio la Marekani eti la kusimamisha vita huko Gaza, mbinu ya kugeuza maoni ya umma
Mar 15, 2024 12:55Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amezungumzia matukio ya hivi karibuni katika eneo la Asia Magharibi hususan Ukanda wa Gaza na kueleza kuwa hakuna anayeamini madai ya Washington ya kujaribu kusimamisha vita vya Gaza.
-
Kurefushwa hali ya hatari kitaifa; muendelezo wa mtazamo wa uadui wa Marekani dhidi ya Iran
Mar 14, 2024 23:17Siku ya Jumanne, Rais Joe Biden wa Marekani alirefusha kwa mwaka mwingine mmoja, muda wa hali ya hatari ya kitaifa kuhusu Iran. Tangu 1995, marais wote wa Marekani wamekuwa wakirefusha kila mwaka hali hiyo iliyoanza kutekelezwa kupitia Agizo la Utendaji nambari 12957 dhidi ya Iran.