-
Morocco yapinga pendekezo la Misri kuhusu Libya
Jun 08, 2020 07:34Serikali ya Morocco imepinga mpango wa Misri kuhusu Libya na kusisitiza kuwa muafaka wa kisiasa wa al Sakhirat ni marejeo asili ya ufumbuzi wa mgogoro wa Libya.
-
Waziri wa zamani wa Misri: Israel ni adui wa kiistratajia wa Wamisri
Jun 07, 2020 22:08Waziri wa zamani wa Misri ameutaja utawala wa Kizayuni wa Israel kama adui wa kistratajia wa wananchi wa nchi hiyo ya Kiarabu ya kaskazini mwa Afrika.
-
Ethiopia yaituhumu Misri kuwa imechochea ghasia na machafuko nchini humo
Jun 04, 2020 07:13Afisa wa serikali ya jimbo la Oromia nchini Ethiopia ameituhumu serikali ya Misri kuwa imechochea maandamano na ghasia zilizoshuhudiwa katika siku za hivi karibuni jimboni humo.
-
Safari ya Jenerali Haftar nchini Misri
Jun 04, 2020 03:19Kamanda wa kundi linalojiita Jeshi la Kitaifa la Libya yuko mjini Cairo Misri, kwa lengo la kuonana na kuzungumza na viongozi wa nchi hiyo.
-
Magaidi 21 waliopanga kuvuruga sherehe za Iddi wauawa Sinai, Misri
May 24, 2020 05:15Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri imetangaza habari ya kuuawa wanachama 21 wa genge moja la kigaidi katika operesheni mbili tofauti zilizofanyika katika Peninsula ya Sinai.
-
Makabila ya kaskazini mwa Misri yajiandaa kutekeleza operesheni dhidi ya ISIS
May 16, 2020 21:50Duru za kieneo zimeripoti kwamba makabila ya eneo la Sinai, kaskazini mwa Misri yametangaza utayarifu wao wa kutekeleza operesheni dhidi ya magaidi wa kundi la Daesh baada ya kumalizika mwezi wa Ramadhani.
-
Wananchi wa Misri wahimiza kupambana na vikwazo vya Marekani dhidi ya Syria
May 10, 2020 03:16Harakati moja ya wananchi wa Misri imesisitiza kuwa, jamii ya kimataifa ina wajibu wa kuishukuru Syria kwa kusimama kidete na kujitolea kupambana vilivyo na magenge ya kigaidi ambayo ni hatari kwa usalama wa dunia nzima, na imeyataka mataifa ya dunia kuungana kupinga vikwazo vya kidhulma vya Marekani dhidi ya Syria.
-
'Rais wa Misri analitumia vibaya janga la corona kujiongezea mamlaka ili kushadidisha ukandamizaji'
May 09, 2020 03:07Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limekosoa hatua ya Rais Abdel Fattah el Sisi wa Misri ya kujiongezea mamlaka kwa kutumia kisingizio cha kukithiri maambukizi ya corona nchini humo.
-
Ushirikiano wa Hamas na Misri katika kukakbiliana na magaidi wakufurishaji eneo la Sinai
May 05, 2020 23:43Duru mjini Cairo zinadokeza kuwa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) inashirikiana na serikali ya Misri katika kukabiliana na magaidi wakufurishaji katika eneo la Sinai.
-
Magaidi 126 na askari 15 wauawa katika mapigano makali Misri
May 03, 2020 21:57Jeshi la Misri limesema askari wake 15 wameuawa katika mapigano makali na magaidi ambapo magaidi 126 wakufurishaji pia wameuawa mashariki mwa nchi.