-
Qassemi: Tuhuma za Morocco dhidi ya Iran zinalenga kuufurahisha upande wa tatu
May 24, 2018 14:38Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: kitendo cha viongozi wa Morocco cha kushupalia na kukariri madai ya uongo kwa ajili ya kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Iran na kuendelea kila mara kuzusha tuhuma zisizo na msingi hakufanyiki kwa lengo jengine zaidi ya kutaka kuzifurahisha baadhi ya pande za tatu.
-
Wananchi wa Morocco waandamana kulaani kuhamishiwa Quds ubalozi wa Marekani
May 21, 2018 07:57Makumi ya maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano katika mji wa Dār al-Bayḍā (Casablanca) kulaani hatua ya Marekani ya kuuhamishia Quds ubalozi wake uliokuweko Tel Aviv, mji mkuu wa utawala pandikizi wa Israel.
-
UN yazitaka Morocco na Polisario kuvumiliana
May 20, 2018 14:22Mgogoro baina ya serikali ya Morocco na harakati ya Polisario inayopigania uhuru wa eneo la Sahara Magharibi umemlazimisha Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuzitaka pande hizo mbili kustahamiliana na zijiepushe na jambo lolote linaloweza kuzusha machafuko katika eneo hilo.
-
Qassemi: Iwapo Marekani itajitoa katika JCPOA, itapata pigo kubwa
May 07, 2018 15:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, iwapo Marekani itajitoa katika mapatano ya nyuklia yanayojulikana kwa kifupi kama JCPOA, basi madhara yake yataikumba Washington yenyewe kabla ya upande mwingine wowote.
-
Iran: Madai ya Morocco kuwa tunaiunga mkono Polisario hayana msingi
May 02, 2018 15:24Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekadhibisha vikali madai yaliyotolewa na serikali ya Morocco kwamba Tehran inawapatia misaada wapiganaji wa harakati ya Polisario inayopigania kujitenga eneo la Sahara Magharibi.
-
Serikali ya Morocco yatoa sharti kwa POLISARIO la mazungumzo kwa ajili ya Sahara Magharibi
Apr 28, 2018 16:12Mwakilishi wa Morocco katika Umoja wa Mataifa amesema Harakati ya Ukombozi wa Sahara Magharibi POLISARIO itaweza kushiriki kwenye mazungumzo na mchakato wa kisiasa kwa sharti kwamba iondoke kwenye eneo la uzio wa Sahara Magharibi.
-
Morocco yaondoa ndege zake za kivita katika muungano wa Saudia dhidi ya Yemen
Apr 16, 2018 04:11Morocco inapanga kuondoa ndege zake za kivita zilizoko katika muungano wa Saudi Arabia ambao umekuwa ukiihujumu Yemen kwa zaidi ya miaka mitatu sasa.
-
Spika wa Bunge la Morocco alaani ukatili wa Israel Ukanda wa Gaza
Apr 06, 2018 04:35Spika wa Bunge la Morocco amesema kuwa vitendo vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Morocco yaitaka UN na Algeria kubeba dhima ya harakati za Polisario
Apr 05, 2018 07:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco ameutaka Umoja wa Mataifa na taifa la Algeria kubeba dhima ya mashambulizi ya Harakati ya Kupigania Ukombozi wa Sahara Magharibi Polisario.
-
Morocco kuimarisha ulinzi mipakani kukabiliana na magendo ya binadamu na ugaidi
Feb 18, 2018 15:56Vyombo vya habari vya nchini Morocco vimetangaza kuwa, Rabat ina nia ya kuanzisha vituo 10 vipya vya kusimamia na kudhibiti maeneo ya mpakani mwa nchi hiyo na Algeria.