-
Umoja wa Afrika walaani mashambulizi dhidi ya Niger; waahidi kuiunga mkono nchi hiyo
Feb 01, 2026 07:04Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mahmoud Ali Youssouf amelaani mashambulizi ya hivi karibuni huko Niger ikiwa ni pamoja na shambulio kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamani Diori katika mji mkuu Niamey. Ali Youssouf amesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba Umoja wa Afrika uko pamoja na Niger.
-
Jeshi la Niger lasema zaidi ya magaidi 70 "wameangamizwa"
Jan 28, 2026 13:19Jeshi la Niger limesema kwamba, zaidi ya magaidi 70 "waliangamizwa" kote nchini kati ya Januari 19 na 25, wakiwemo zaidi ya 50 waliouawa katika mashambulizi ya anga yaliyolenga "mikusanyiko ya maadui."
-
Polisi 10 wauawa katika shambulio kwenye kituo cha polisi Niger
Jan 28, 2026 02:31Askari polisi wasiopungua 10 wa Niger wameuawa wakati watu wenye silaha waliposhambulia kituo cha polisi kaskazini mwa nchi hiyo. Eneo la kaskazini mwa Niger limekumbwa na machafuko ya magenge ya wahalifu wenye silaha.
-
Mali, Burkina Faso na Niger zaanzisha kituo cha Televisheni kukabiliana na taarifa za upotoshaji
Dec 24, 2025 06:17Viongozi wa Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES), kundi linalojumuisha Mali, Burkina Faso na Niger, umeanzisha shirika jipya la habari lenye makao yake makuu katika mji mkuu wa Mali, Bamako.
-
Serikali ya Nigeria yafanikisha kuachiwa huru watoto 100 waliotekwa nyara katika jimbo la Niger
Dec 08, 2025 06:26Serikali ya Nigeria imefanikisha kuachiliwa huru watoto 100 wa skuli waliotekwa nyara mwezi uliopita katika Jimbo la Niger. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na televisheni ya Channels Television jana Jumapili.
-
Je, kujitawala kiuchumi Niger kutakuwa pigo la mwisho kwa ukoloni wa Ufaransa barani Afrika?
Dec 03, 2025 09:14Niger imeanza kuuza urani yake katika soko la kimataifa baada ya kukata mkono wa Ufaransa katika sekta ya madini hayo nchini humo.
-
Niger katika Mkutano wa UNGA: Ufaransa inapasa kukumbuka na kutambua jinai zake
Sep 28, 2025 07:02Lamine Zeine Ali Mahaman Waziri Mkuu wa serikali ya mpito ya Niger ameikosoa Ufaransa nchi mkoloni wa zamani wa nchi hiyo akisema kuwa nchi hiyo ya Ulaya inatumia ugaidi kudhoofisha taifa hilo la eneo la Sahel.
-
Makumi waaga dunia kwa mafuriko nchini Niger, maelfu waathirika
Aug 21, 2025 05:42Kwa uchache watu 47 wamepoteza maisha, huku zaidi ya 56,000 wakilazimika kuhama makazi yao kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha hivi majuzi nchini Niger.
-
Makamanda 11 wa ugaidi wauawa katika operesheni za jeshi la Nigeria
May 08, 2025 07:04Takriban vinara 11 wa magenge ya kigaidi nchini Nigeria wameuawa na vikosi vya serikali katika operesheni za kupambana na ugaidi katika nchi hiyo yenye watu wengi zaidi barani Afrika.
-
Aref: Msingi wa kuimarika uhusiano wa Iran, Niger ni Mapinduzi ya Kiislamu
Apr 30, 2025 02:33Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad-Reza Aref amesema Jamhuri ya Kiislamu imekuwa ikitekeleza sera yake ya kukuza uhusiano na Niger na mataifa mengine ya bara la Afrika kwa kuzingatia thamani na maadili ya Mapinduzi ya Kiislamu.