-
UN: Kutoadhibiwa wahalifu kunaeneza hisia za mauaji ya kimbari nchini Nigeria
Jun 21, 2026 02:52Ripoti ya Umoja wa Mtaifa inasema, kutoadhibiwa watu wanaofanya mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya viongozi wa kidini na sehemu za ibada, pamoja na kinga dhaifu na uwajibikaji duni, vinawafanya waathiriwa nchini Nigeria kuona kwamba vurugu zinazofanyika nchini humo ni mateso au hata mauaji ya halaiki.
-
Nigeria: Karibu wapiganaji 10,000 wa zamani wa Boko Haram waunganishwa katika jamii
Jun 16, 2026 11:00Mamlaka husika katika Jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria zimearifu kuwa karibu wapiganaji 10,000 wa zamani wa kundi la waamgambo wa Boko Haram sasa wameunganishwa tena katika jamii chini ya mpango unaofadhiliwa na serikali wa kurekebisha tabia na kuhimiza kuachana na makundi ya uasi.
-
Rais wa Nigeria atangaza mauaji ya wapiganaji 13,000 mwaka jana
Jun 12, 2026 12:36Rais wa Nigeria, Bola Ahmed Tinubu, ametangaza leo Ijumaa kwamba "magaidi" wasiopungua 13,000 waliuawa nchini Nigeria mwaka jana, akisisitiza kwamba idadi ya vifo vinavyotokana na uasi wa kutumia silaha nchini humo imepungua kwa 81% tangu alipochukua madaraka Mei 2023.
-
Nigeria: Mamia ya wanawake na watoto waliotekwa nyara na magaidi waachiliwa
Jun 08, 2026 03:12Mamia ya wanawake na watoto waliokuwa wametekwa nyara na kundi la kigaidi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria wameachiwa huru mwishoni mwa wiki.
-
Jeshi la Nigeria laangamiza magaidi 50, yumo kamanda mkuu wa kundi la ISWAP
Jun 04, 2026 03:05Wanajeshi wa Nigeria wanaoendesha oparesheni kwa jina "Hadin Kai" wamewaangamiza magaidi wasiopungua 50, akiwemo kamanda mkuu wa tawi la ISWAP lililoungana na kundi la Boko Haram.
-
Walimu Nigeria waitisha mgomo katika jimbo la Oyo kufuatia vitendo vya utekaji nyara shuleni
Jun 02, 2026 02:53Muungano wa Walimu wa Nigeria umeitisha mgomo wa wazi kuanzia leo Jumatatu katika jimbo la Oyo kupinga kutekwa nyara makumi ya watoto na walimu wao katikati ya mwezi wa Mei mwaka huu.
-
Watu wenye silaha wawateka nyara makumi ya wanafunzi katika Jimbo la Borno nchini Nigeria
May 17, 2026 02:34Watu waliokuwa na silaha wameteka nyara makumi ya wanafunzi wa shule katika jimbo lililokumbwa na machafuko la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Baada ya Ghana, Nigeria pia yamwita balozi wa Afrika Kusini kuhusu mashambulizi ya chuki dhidi ya wageni
May 03, 2026 10:12Wimbi jipya la mashambulizi ya chuki dhidi ya wageni, linalowalenga wahamiaji wa Kiafrika na biashara zao huko Afrika Kusini linatishia kuteteresha uhusiano wa nchi hiyo na nchi nyingine za Afrika.
-
Sheikh Zakzaky: Jina la kiongozi aliyeuawa shahidi wa Iran limekuwa membo ya mapambano
Apr 26, 2026 09:23Sheikh Ibrahim Zakzaky, kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria, amemtaja Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, kiongozi aliyeuawa shahidi wa Iran, kuwa ni nembo mapambano, imani na kusimama kidete.
-
Jeshi la Nigeria lauwa magaidi 25 na kuzima njama yao kaskazini mashariki mwa nchi
Apr 25, 2026 05:24Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limeuwa magaidi 25, akiwemo kamanda wao wa ngazi ya juu katika hujuma ya magaidi hayo iliyozimwa na jeshi dhidi ya jamii moja kaskazini mashariki mwa Nigeria.