-
Harakati ya Kiislamu ya Nigeria yataka kuachiliwa wanaharakati wa Sumud
Oct 10, 2025 06:25Harakati ya Kiislamu ya Nigeria imelaani kitendo cha utawala wa Kizayuni cha kuendelea kuwashikilia wanaharakati wa msafara wa kimataifa wa meli nyingi wa Sumud uliokuwa ukielekea Ukanda wa Gaza, na kutaka kuachiwa mara moja kwa raia wa Nigeria na wa mataifa mengine waliotekwa nyara na kuzuiliwa na askari wa majini wa Kizayuni.
-
Wanigeria waandamana kulaani shambulio la Israel dhidi ya msafara wa Sumud
Oct 04, 2025 06:04Waislamu kote nchini Nigeria waliingia barabarani baada ya Swala ya Ijumaa hapo jana kulaani shambulio la Israel dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumud, wenye makumi ya meli zinazoelekea katika Ukanda wa Gaza.
-
Jumatano, Oktoba Mosi, 2025
Oct 01, 2025 02:31Leo ni Jumatano tarehe 8 Mfunguo Saba Rabiul-Thani 1447 Hijria Qamaria, sawa na tarehe 9 Mehr mwaka 1404 Hijria Shamsia, inayosadifiana na tarehe Mosi Oktoba 2025 Miladia.
-
Wafanyakazi wa sekta ya mafuta Nigeria waendelea na mgomo wakipinga kupunguzwa wafanyakazi katika kiwanda cha Dangote
Sep 30, 2025 11:58Ofisi za idara ya Udhbiti wa Mafuta na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Nigeria zimefungwa kutokana na mgomo wa kitaifa ulioanzishwa na jumuiya ya wafanyakazi wa sekta ya mafuta baada ya kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote kuwafuta kazi zaidi ya wafanyakazi 800.
-
Polisi 3 wauawa na 7 watekwa nyara katika hujuma ya wanamgambo wenye silaha Nigeria
Sep 22, 2025 09:08Maafisa watatu wa polisi wameuawa na wengine saba kutekwa nyara jana Jumapili katika shambulio la wanamgambo wenye silaha katika Jimbo la Benue nchini Nigeria.
-
Kuanzia kupambana na ubaguzi wa rangi hadi kushirikiana na wavamizi; Nigeria inaelekea wapi?
Sep 19, 2025 15:07Nigeria imesimama na mataifa yanayodhulumiwa katika miongo kadhaa iliyopita, hasa katika mapambano dhidi ya utawala wa kibaguzi nchini Afrika Kusini, na imetetea misingi ya haki na kupinga ukoloni.
-
CEDAW: Nigeria ina dhima ya ukiukaji mkubwa na wa kimfumo wa haki za wanawake waliotekwa nyara
Sep 18, 2025 03:44Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) imesema, serikali ya Nigeria inawajibika kwa ukiukaji mkubwa na wa kimfumo wa haki za wanawake na wasichana katikati ya matukio ya utekaji wa watu wengi
-
Ajali nyingine ya boti yaua watu zaidi ya 60 nchini Nigeria
Sep 04, 2025 07:43Kwa akali watu 60 wamefariki dunia baada ya mashua iliyokuwa imebeba zaidi ya abiria 100 kupinduka na kuzama katika jimbo la Niger, kaskazini mwa Nigeria.
-
Waislamu Nigeria wataka kuachiwa huru kiongozi wa Palestina
Aug 29, 2025 02:24Harakati ya Kiislamu ya Nigeria imelaani vikali hatua ya polisi ya Nigeria kumkata kiongozi wa Jumuiya ya Wapalestina katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi, Ramzy Abu Ibrahim, ikisisitiza kuwa kukamatwa huko kunafungamana na makubaliano ya hivi karibuni ya usalama kati ya Nigeria na utawala wa Israel.
-
Kampuni ya Mafuta ya Serikali ya Nigeria: Wizi wa mafuta kupitia mabomba wakaribia kukomeshwa
Aug 26, 2025 02:45Kampuni ya mafuta ya serikali ya Nigeria (NNPC Limited) imeripoti kuwa karibu wizi wote wa mafuta uliokuwa ukifanywa kupitia mabomba umekaribia kukomeshwa, baada ya juhudi zilizoratibiwa na mashirika ya ulinzi na intelijensia ya nchi hiyo.