-
Katibu Mkuu wa UN ataka India, Pakistan zipunguze uhasama
Feb 20, 2019 04:31Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa India na Pakistan zichukue hatua za haraka kupunguza uhasama baina yao kufuatia hujuma mbaya ya kigaidi huko Kashmir ambayo imepelekea kuwepo hatari ya kuibuka mapigano baina ya nchi hizo mbili zenye silaha za nyuklia.
-
India yaituhumu Pakistan kwa kuhusika na shambulizi la Kashmir
Feb 19, 2019 12:21Kamanda wa jeshi la India katika eneo la Kashmir Luteni Jenerali G S Dhillon amesema kuwa shirika la ujasusi la Pakistan limehusika katika hujuma iliyolenga msafara wa askari usalama wa nchi hiyo wiki iliyopita ambayo imeua zaidi ya askari 40 wa India.
-
Bahram Qassemi: Madola ya Ulaya hayapaswi kufuatilia kukamilisha matakwa yao kutoka kwa Iran
Feb 18, 2019 11:44Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, subira na uvumilivu wa wananchi na serikali ya Iran una mipaka na kwamba, madola ya Ulaya hayapaswi kutumia muda kwa ajili ya kufuatilia kukamilisha matakwa yao kutoka kwa Iran.
-
Safari ya Bin Salman nchini Pakistan, mgeni aliyesusiwa na wenyeji
Feb 18, 2019 07:29Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia, Muhammad bin Salman aliwasili jana Jumapili nchini Pakistan akiandamana na ndege saba na akisindikizwa na ndege kadhaa za kijeshi za Pakistan. Safari hiyo inafanyika chini ya ulinzi mkali.
-
Mazungumzo ya Waziri Mkuu wa Pakistan na viongozi wa Qatar mjini Doha
Jan 22, 2019 23:17Katika safari yake ya kwanza rasmi nchini Qatar, Waziri Mkuu wa Pakistan Jumatatu usiku alikutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Abdullah bin Nasser bin Khalifa Al Thani.
-
Takwa la Pakistan kwa Taliban la kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na serikali ya Afghanistan
Jan 12, 2019 23:26Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Pakistan amelitaka kundi la wanamgambo wa Taliban kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na serikali ya Afghanistan bila ya kupitia kwa mtu mwingine ili kufanikisha malengo ya amani.
-
Jibu la Pakistan kwa matamshi ya hivi karibuni ya Waziri Mkuu wa India
Jan 04, 2019 04:33Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Pakistan amelaani vikali vitisho na matamshi yaliyotolewa hivi karibuni ya Waziri Mkuu wa India dhidi ya Pakistan.
-
Sisitizo la maulamaa wa Pakistan la kuwa kitu kimoja Waislamu wa Kishia na Kisuni
Dec 22, 2018 21:36Maulamaa wa Kishia na Kisuni wa Pakistan wametilia mkazo kuwepo umoja kati ya Waislamu nchini humo ili kukabiliana na njama za maadui wa Uislamu.
-
Rouhani: Madola ya kibeberu ndiyo yaliyounda makundi ya kigaidi duniani
Dec 09, 2018 00:05Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema madola ya kibeberu ndiyo yaliyounda na kuyafadhili kwa hali na mali makundi ya kigaidi duniani, na kwamba irada thabiti na jitihada za pamoja zinahitajika ili kulitokomeza jinamizi hilo linalotishia usalama wa dunia.
-
Mkutano wa maspika wa mabunge ya nchi sita wamalizika mjini Tehran kwa kutoa taarifa
Dec 08, 2018 12:07Maspika wa mabunge ya nchi sita za Iran, Russia, Uturuki, China, Pakistan na Afghanistan umemalizika leo hapa mjini Tehran kwa taarifa ya pamoja ya kuimarisha uhusiano katika kupambana na ugaidi na kuongeza ushirikiano wao wa kieneo.