-
Wananchi wa Iran wasisitiza kuhusu kukombolewa Quds Tukufu
Jun 08, 2018 09:12Wananchi wa Iran walioshiriki katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds wametoa taarifa na kusisitiza kuhusu kukombolewa Quds (Jerusalem) Tukufu na kujikomboa Wapalestina wanaodhulumiwa kutoka katika makucha ya utawala ghasibu wa Israel.
-
Velayati: Muqawama wa Palestina umeidhoofisha mno Israel
Jun 08, 2018 02:57Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema harakati za muqawama wa Palestina zimeudhoofisha utawala wa Kizayuni, na kuandaa mazingira ya kupata ushindi mkubwa dhidi ya Tel Aviv.
-
(Hatua kwa Hatua Hadi Siku ya Quds) Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu kuhusu umuhimu wa Siku ya Kimataifa ya Quds
Jun 08, 2018 01:38Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Jumatatu ya wiki hii alitoa hotuba muhimu katika Haram ya Imam Khomeini MA, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambapo moja ya nukta muhimu zilizojikita kwenye hotuba yake hiyo ni kadhia ya Palestina na hasa Siku ya Kimataifa ya Quds ambayo inaadhimishwa leo Ijumaa kote ulimwenguni.
-
Imam wa msikiti wa Al-Aqsa: Macho ya walimwengu yameelekezwa kwenye Siku ya Kimataifa ya Quds
Jun 08, 2018 00:06Imam na Khatibu wa msikiti wa Al-Aqsa amesisitiza kuwa mamlaka ya msikiti huo yatabaki kuwa mikononi mwa Waislamu na kwamba wanaovamia na kukivunjia heshima kibla hicho cha kwanza cha Waislamu hawatopata faida yoyote.
-
Marekani, Israel, Saudia zachochea machafuko Jordan kwa kupinga kuhamishiwa ubalozi wa Marekani mjini Quds
Jun 05, 2018 22:04Gazeti moja la utawala wa Kizayuni wa Israel limefichua kuwa, Israel, Marekani, Saudi Arabia na baadhi ya nchi nyingine za Kiarabu zinahusika katika machafuko yanayoendelea nchini Jordan kutokana na nchi hiyo kushiriki katika kikao cha kupinga kuhamishiwa Quds ubalozi wa Marekani uliokuweko Tel Aviv.
-
Siku ya Kimataifa ya Quds Kufanyika Nairobi, Kenya
Jun 04, 2018 23:21Wapenda haki na amani nchini Kenya watajiunga na wenzao kote duniani katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds Ijumaa wiki hii.
-
Waziri wa vita wa Israel atoa vitisho vipya kwa Wapalestina
Jun 04, 2018 22:36Waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni ametishia kuwa Israel itamalizia hasira zake kwa harakati za Hamas, Jihadul Islam na makundi yote ya muqawama ya Palestina yanayoendesha mapambano dhidi ya utawala vamizi wa Kizayuni.
-
Ushindi wa Palestina; utukufu wa ulimwengu wa Kiislamu
Jun 04, 2018 03:52Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kistatijia cha Taasisi ya Kimataifa ya Mweamko wa Kiislamu amesema kwamba ushindi wa taifa la Palestina dhidi ya utawala haramu wa Isreal unauletea utukufu ulimwengu wa Kiislamu.
-
Hizbullah: Taifa la Palestina litegemee muqawama, lisiwategemee viongozi wa Kiarabu wanafiki
Jun 03, 2018 23:46Mjumbe wa Baraza Kuu la Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah, Nabil Qaouk amesisitiza kwamba, taifa la Palestina halitakiwi kuwategemea viongozi wa nchi za Kiarabu na vikao vyao, bali wategemee muqawama na stratijia yake.
-
Zarif: Kitendo cha Israel kumuua muuguzi wa Kipalestina ni fedha juu fedheha
Jun 03, 2018 02:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kitendo cha utawala wa Kizayuni wa Israel cha kumuua shahidi muuguzi wa Kipalestina katika Ukanda wa Ghaza, na kuutaja ukatili huo kama doa jingine kwa utawala huo haramu.