-
Brigedi za al Qassam zasambaratisha vifaru vinne vya merkava vya Israel
Jan 04, 2025 07:49Brigedi za al Qassam zimetangaza mapema leo kuwa zimevisambaratisha vifaru vinne vya merkava vya utawala wa Israel katika oparesheni iliyofanyika mashariki mwa mji wa Jabalia. Brigedi za al Qassam zimevisambaratisha vifaru hivyo kwa kutumia mada za milipuko.
-
NGO: Israel inashikilia miili ya Wapalestina 198 waliouawa mwaka 2024
Jan 01, 2025 13:02Kampeni ya Kitaifa ya Kurejesha Miili ya Mashahidi (The National Campaign to Retrieve Martyrs' Bodies) imeeleza kuwa viongozi wa utawala ghasibu wa Israel wanashikilia miiili ya mashahidi wa Kipalestina 198 walisajiliwa mwaka jana wa 2024.
-
Himaya ya wananchi katika Ulimwengu wa Kiislamu kwa muqawama wa Palestina
Jan 01, 2025 07:38Mwaka mpya wa Miladia wa 2025 umeanza katika ulimwengu wa Kiislamu kwa himaya na uungaji mkono mkubwa wa wananchi kwa makundi ya wapiganaji wa Palestina na viongozi wa muqawama.
-
Riyadh Mansour na Francesca Albanese shakhsia muhimu wa UN kwa mwaka 2024
Dec 29, 2024 12:28Duru za habari zimeripoti kuwa, Mwakilishi wa Kudumu wa Palestina katika Umoja wa Mataifa na Ripota Maalumu wa umoja huo kuhusu masuala ya Palestina wamechaguliwa kuwa shakhsia muhimu wa Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2024.
-
Mielekeo tofauti inayoonyeshwa na nchi za Ulaya kuhusiana na jinai za Wazayuni inaashiria nini?
Dec 27, 2024 03:00Wakati Waziri Mkuu wa Ireland Simon Harris amesisitiza kwa mara nyingine tena mshikamano wa nchi yake na Palestina na kuyataja mauaji ya Wapalestina kuwa ni "utovu wa hisia za dhamiri na janga la kibinadamu", mkabala na matamshi hayo, serikali ya Ujerumani imetoa kibali cha kusafirisha na kuipelekea silaha Israel.
-
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran: Muqawama wa Wapalestina umeonyesha sura halisi ya mfumo wa kibeberu
Dec 23, 2024 03:11Kamanda Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, muqawama wa Palestina na Mujahidina wa Gaza wameonyesha sura mbaya na ya kweli ya mfumo wa kibeberu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Mamia ya maelfu ya Wayemen wafanya maandamano ya kuiunga mkono Palestina
Dec 21, 2024 02:56Mamia ya maelfu ya wananchi wa Yemen kwa mara nyingine tena wamemiminika barabarani kufanya maandamano makubwa ya kuwaunga mkono wananchi wa Palestina na kuupinga utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Jeshi la Kizayuni lamuua Babu mtu wa Kipalestina aliyegusa nyoyo za walimwengu mitandaoni
Dec 17, 2024 06:05Shambulio la kinyama la makombora lililofanywa na jeshi la Kizayauni katika Ukanda wa Ghaza limemuua Khaled Nabhan, Mpalestina ambaye amefahamika sana kwenye mitandao ya kijamii kutokana na video iliyomuonyesha akibusu macho ya mjukuu wake aliyeuliwa na kumwita "roho ya roho yangu".
-
Ripoti ya kila mwaka ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na Marekani na Uingereza
Dec 16, 2024 06:52Kwa mujibu wa ripoti ya kila mwaka ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusiana na ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa Marekani na Uingereza, ripoti ambayo imeandaliwa kwa kutelekeza mswada uliopitishwa na Bunge la Iran mwaka 1391 Hijria Shamsia,
-
Droni za Yemen zahepa mifumo ya utunguaji ya utawala wa Kizayuni, zapiga Tel Aviv na Ashkelon
Dec 14, 2024 06:27Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza kuwa vimefanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani kulenga mji wa Jaffa karibu na Tel Aviv pamoja na mji wa Ashkelon katika eneo la kati la ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu katika operesheni mpya dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.