-
"Kuna haja ya kuitetea Gaza katika Hija ya mwaka huu"
May 17, 2024 07:10Rais wa Chuo cha Da'awa ya Kiislamu cha Lebanon amesema ibada ya Hija ya mwaka huu ina umuhimu wa kipekee wakati huu ambapo Wazayuni wanaendelea kumwaga damu za Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, "Kuna haja ya kuitetea Gaza katika Hija ya mwaka huu."
-
AFC yataka FIFA iifutie uanachama Israel kutokana na jinai zake Gaza
May 16, 2024 12:21Shirikisho la Soka Asia (AFC) limetangaza kuunga mkono ombi la Palestina la kulitaka Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) liifutie uanachama Israel katika taasisi hiyo kubwa zaidi ya kandanda duniani, kutokana na utawala huo wa Kizayuni kutenda jinai kubwa dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Ireland kuitambua rasmi nchi huru ya Palestina
May 16, 2024 07:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland amesema kuwa, mnamo siku chache zijazo, Dublin itaitambua rasmi nchi huru ya Palestina.
-
Maelfu ya Wapalestina waandamana katika kumbukumbu ya siku ya Nakba
May 15, 2024 13:37Maelfu ya wananchi wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu wameandamana kwa mnasaba wa Siku ya Nakba ambayo inakumbusha uvamizi, mauaji ya kimbari, ukatili na jinai za Wazayuni katika ardhi za Wapalestina.
-
Iran: Israel ni nembo ya ugaidi ulioratibiwa duniani
May 14, 2024 11:57Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imeutaja utawala wa Kizayuni wa Israel kama nembo kuu ya ugaidi ulioratibiwa duniani.
-
Makumi ya Wapalestina wauawa katika hujuma za Israel Gaza
May 14, 2024 11:05Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel zimefanya mashambulizi mapya ya anga dhidi ya maeneo tofauti ya Ukanda wa Gaza na kuua shahidi makumi ya Wapalestina, wakiwemo watoto wadogo na wanawake.
-
Maandamano ya kuunga mkono Palestina na Ghaza yaendelea katika miji mbalimbali duniani
May 13, 2024 04:04Watu wa miji tofauti katika nchi mbalimbali duniani, kwa mara nyingine wamemiminika mabarabarani wakiandamana kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina hususan wa Ukanda wa Ghaza na kulaani jinai za mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala dhalimu wa Kizayuni wa Israel katika eneo hilo.
-
Borrel asema uhamisho hauvumiliki; aikosoa Israel kwa kuwahamisha kwa lazima Wapalestina katika mji wa Rafah
May 12, 2024 12:16Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amelaani na kuitaja kuwa isiyovumilika hatua ya utawal wa Israel ya kuwaondoa kwa lazima raia wa Kipalestina katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza. Utawala wa kizayuni umechukua hatua hii huku ukijiandaa kuanzisha mashambulizi makubwa ya ardhini katika mji huo.
-
Iran: Israel haijawahi kutengwa kiasi hiki katika historia yake bandia
May 12, 2024 03:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameashiria hatua ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA ya kupasisha rasimu ya azimio la kutaka kutazamwa upya suala la taifa la Palestina kupewa uanachama kamili katika umoja huo na kusema kuwa, utawala haramu wa Israel haujawahi kutengwa kwa kiwango kikubwa kama cha sasa katika historia yake bandia.
-
Afisa wa Hamas: Muqawama wa Gaza umeweza kukabiliana kwa mafanikio na vita vya dunia
May 12, 2024 02:36Sami Abu Zuhri, ambaye ni miongoni mwa viongozi wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS), amesema kwamba Muqawama na mapambano ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza yamefanikiwa kukabiliana na "vita vya kimataifa," na nchi zilizoifadhili Israel sasa zinaanza kusitisha uungaji mkono wao kwa utawala huo.