-
Upinzani wa Marekani dhidi ya hatua ya nchi za Ulaya ya kulitambua taifa la Palestina
May 24, 2024 04:25Siku ya Jumatano, Ikulu ya Marekani ailitoa taarifa ya kuunga mkono kwa pande zote utawala haramu Israel na kusema kuwa Rais Biden anaamini kwamba taifa la Palestina linapaswa kuanzishwa kupitia mazungumzo na si kutambuliwa kwa upande mmoja na baadhi ya nchi.
-
Waarabu wazipongeza nchi za Ulaya zilizolitambua taifa la Palestina
May 23, 2024 06:58Mataifa ya Kiarabu yamekaribisha hatua ya baadhi ya nchi za Ulaya ya kutangaza rasmi kulitambua taifa la Palestina.
-
Ansarullah: Shahidi Raisi aliitetea Palestina hadi siku za mwisho kabisa za uhai wake
May 23, 2024 04:15Msemaji wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen Muhammad Abdussalam amesema, Shahidi Sayyid Ebrahim Raisi aliitetea Palestina hadi siku za mwisho kabisa za uhai wake.
-
Polisi wa Marekani wawapiga na kuwatia nguvuni watetezi wa Palestina walioadhimisha Siku ya Nakba
May 19, 2024 07:45Askari polisi wa Marekani wamewapiga na kuwakamata watu kadhaa katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaliyofanyika katika mji wa Brooklyn jimboni New York, ukiwa ni mwendelezo wa operesheni za kukandamiza na kuzima sauti zinazopinga vita dhidi ya Ghaza nchini Marekani.
-
"Kuna haja ya kuitetea Gaza katika Hija ya mwaka huu"
May 17, 2024 03:40Rais wa Chuo cha Da'awa ya Kiislamu cha Lebanon amesema ibada ya Hija ya mwaka huu ina umuhimu wa kipekee wakati huu ambapo Wazayuni wanaendelea kumwaga damu za Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, "Kuna haja ya kuitetea Gaza katika Hija ya mwaka huu."
-
AFC yataka FIFA iifutie uanachama Israel kutokana na jinai zake Gaza
May 16, 2024 08:51Shirikisho la Soka Asia (AFC) limetangaza kuunga mkono ombi la Palestina la kulitaka Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) liifutie uanachama Israel katika taasisi hiyo kubwa zaidi ya kandanda duniani, kutokana na utawala huo wa Kizayuni kutenda jinai kubwa dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Ireland kuitambua rasmi nchi huru ya Palestina
May 16, 2024 03:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland amesema kuwa, mnamo siku chache zijazo, Dublin itaitambua rasmi nchi huru ya Palestina.
-
Maelfu ya Wapalestina waandamana katika kumbukumbu ya siku ya Nakba
May 15, 2024 10:07Maelfu ya wananchi wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu wameandamana kwa mnasaba wa Siku ya Nakba ambayo inakumbusha uvamizi, mauaji ya kimbari, ukatili na jinai za Wazayuni katika ardhi za Wapalestina.
-
Iran: Israel ni nembo ya ugaidi ulioratibiwa duniani
May 14, 2024 08:27Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imeutaja utawala wa Kizayuni wa Israel kama nembo kuu ya ugaidi ulioratibiwa duniani.
-
Makumi ya Wapalestina wauawa katika hujuma za Israel Gaza
May 14, 2024 07:35Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel zimefanya mashambulizi mapya ya anga dhidi ya maeneo tofauti ya Ukanda wa Gaza na kuua shahidi makumi ya Wapalestina, wakiwemo watoto wadogo na wanawake.