-
Maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaendelea katika miji tofauti duniani
May 01, 2024 03:20Wananchi wa miji tofauti ya dunia kwa mara nyingine wameandamana kuwatetea wananchi madhulumu wa Palestina na kulaani jinai za utawala ghasibu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Vituo vya utafiti vya Ulaya vyaiunga mkono Palestina na kuiwekea vikwazo Israel
Apr 30, 2024 07:41Vituo vya utafiti barani Ulaya vimeuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni na kuunga mkono malengo ya Palestina. Viituo hivyo vya utafiti vya Ulaya pia vimelaani jinai za utawala huo unaotekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Gaza.
-
Wanachuo wanaoitetea Palestina Marekani watiwa nguvuni Texas, wasimamishwa masomo Columbia
Apr 30, 2024 04:18Polisi nchini Marekani wamekabiliana na wanafunzi wa chuo kikuu katika mji wa Austin jimboni Texas, na kuwakamata makumi ya watu baada ya kubomoa mahema yaliyowekwa kupinga na kulalamikia vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ghaza.
-
Arab League: Lengo la Utawala wa Kizayuni ni kuifuta Palestina pamoja na haki zake
Apr 30, 2024 03:52Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amesema, lengo la vita vya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza ni kufuta uwepo wa Palestina na haki zake na vilevile kulifuta moja kwa moja suala la Palestina.
-
Wapalestina zaidi ya 8,500 wametiwa nguvuni Ukingo wa Magharibi tangu Oktoba 7 hadi sasa
Apr 29, 2024 23:16Jumuiya ya kushughulikia mateka wa Kipalestina imetangaza katika ripoti yake kwamba utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel umewatia nguvuni Wapalestina 8,505 katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan tangu tarehe 7 Oktoba 2023 mara baada ya kutekelezwa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
Mgombea wa uchaguzi wa rais Marekani atiwa nguvuni katika maandamano ya watetezi wa Palestina
Apr 28, 2024 23:06Polisi nchini Marekani imemtia nguvuni mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka huu nchini humo ambaye alikuwa katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Washington.
-
Jumatatu, tarehe 29 Aprili, 2024
Apr 28, 2024 23:05Leo ni Jumatatu tarehe 20 Shawwal 1445 Hijria sawa na Aprili 29 mwaka 2024.
-
HAMAS: Msaada mpya wa Marekani kwa Israel ni kwa ajili ya kuendeleza mauaji ya umati
Apr 21, 2024 23:03Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeilaani Marekani kwa kupasisha msaada mwingine kwa utawala wa Kizayuni na kusema kuwa msaada huo ni kwa ajili ya kuendeleza mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Marekani; kizuizi kikuu kwa Palestina kuwa mwanachama kamili katika Umoja wa Mataifa
Apr 20, 2024 08:47Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu wa Israel kwa mara nyingine imetumia kura ya turufu (Veto) na kuzuia kupasishwa uanachama kamili wa Palestina ndani ya Umoja wa Mataifa.
-
Iran yalaani veto ya Marekani dhidi ya uanachama kamili wa Palestina UN
Apr 20, 2024 03:13Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kura ya turufu ya Marekani dhidi ya rasimu ya azimio iliyotaka Palestina ipewe uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.