-
Wapalestina waandamana Ukingo wa Magharibi kuwaunga mkono wenzao wa Ghaza
Oct 11, 2023 04:34Raia wa Palestina wamefanya maadnamano katika maeneo mbalimbali ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kuonyesha uungaji mkono wao kwa wenzao wa Ukanda wa Ghaza sambamba na kuyaunga mkono makundi ya muqawama dhidi ya utawala wa Kizayuni.
-
Iran: Wapalestina wana haki kisheria ya kujihami na uvamizi na kukaliwa ardhi zao na Israel
Oct 10, 2023 23:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, akieleza wasiwasi alionao kuhusu hujuma na jinai za kutisha zinazofanywa na utawala ghasibu wa Israel, na kusisitiza kwamba wananchi wa Palestina wana haki ya kisheria ya kujihami dhidi ya aina yoyote ya uchokozi na kukaliwa ardhi zao kwa mabavu.
-
Vladimir Putin: Wakati umefika wa kutangazwa nchi huru ya Palestina
Oct 10, 2023 23:27Rais Vladimir Putin wa Russia amezungumzia kushindwa siasa za kibeberu za rais wa Marekani, Joe Biden za kuingilia masuala ya eneo la Asia Magharibi na kutilia mkazo wajibu wa kutekelezwa maamizio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanayosisitizia kuundwa nchi huru ya Palestina.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Israel itachapwa "kibao kikali zaidi" kwa mauaji ya halaiki inayofanya Ukanda wa Gaza
Oct 10, 2023 11:08Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema Israel itachapwa "kibao kikali zaidi" kwa mauaji inayoendelea kufanya dhidi ya wananchi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza iliouwekea mzingiro.
-
Ayatullah Sistani: Waislamu wote wana wajibu wa kuwasaidia Wapalestina
Oct 10, 2023 10:39Kiongozi wa juu wa kidini wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq ametoa mwito kwa Waislamu kote duniani kuwaunga mkono, kuwahami na kuwasaidia wananchi wa Palestina, wakati huu ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel unaendelea kufanya mashambulizi ya kikatili dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
-
Iran: Tuko tayari kuongoza mkutano wa nchi za Kiislamu kujadili Palestina
Oct 10, 2023 10:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ipo tayari kuwa mwenyeji wa mkutano wa dharura wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC), kwa ajili ya kuzungumzia kadhia ya Palestina.
-
Mapambano yanaendelea kwa siku ya tatu, Hamas yapiga Ashkelon na Ashdod
Oct 09, 2023 11:33Mapigano kati ya wapigania ukombozi wa Palestina na jeshi la utawala vamizi wa Israel yameendelea leo kwa siku ya tatu katika maeneo ya ndani ya vitongoji vya walowezi wa Kizayuni karibu na Ukanda wa Gaza, ukiwa mwendelezo wa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa iliyoanzishwa na Brigedi za Izzuddin Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (Hamas) dhidi ya uvamizi wa Israeli, huku kukiwa na makadirio kwamba Wazayuni wasiopunguau 1,000 wa Israeli wameangamizwa hadi sasa.
-
Undani wa oparesheni ya Kimbunga cha Al Aqsa kwa upande wa kijeshi na kiitelijinsia
Oct 09, 2023 04:43Makundi ya muqawama ya Palestina yenye makao katika Ukanda wa Ghaza yaani harakati ya Hamas na harakati nyingine za Palestina khususan Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina juzi Jumamosi tarehe 7 Oktoba yalianzisha oparesheni kwa jina la Kimbunga cha Al Aqsa dhidi ya utawala wa Kizayuni; oparesheni iliyouduwaza kikamilifu utawala huo na kuwashtua pakubwa Wazayuni.
-
"Operesheni ya al-Aqsa imegeuza ndoto ya kuporomoka Israel kuwa uhalisia"
Oct 09, 2023 03:50Mkuu wa Komandi Kuu ya Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema ndoto na jinamizi la kuangamia na kupomoka kwa utawala wa Kizayuni wa Israel sasa imegeuka kuwa hali halisi kutokana na Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
Idadi ya vifo vya Wazayuni yaongezeka hadi watu 1000
Oct 09, 2023 02:07Vyombo vya habari vya Kizayuni vimeripoti kuwa, idadi ya Wazayuni waliouawa katika operesheni za hivi karibuni za wapiganaji wa muqawama wa Palestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu imefikia 1000.