-
Rais wa Misri asaini sheria inayowapa kinga majenerali wa jeshi
Jul 27, 2018 03:16Rais Abdul Fattah al-Sisi wa Misri ameidhinisha sheria inayowapa kinga ya kufikishwa mahakamani majenerali wa jeshi wanaohusishwa na machafuko yaliyotokea baada ya mapinduzi ya Rais wa kwanza kuchaguliwa kwa njia za kidemokrasia nchini humo; siku 10 baada ya Bunge la nchi hiyo kupasisha kwa kishindo muswada wa sheria hiyo.
-
Rais wa Ufilipino aidhinisha kuundwa eneo lenye mamlaka ya ndani la Waislamu nchini humo
Jul 27, 2018 03:15Rais Rodrigo Duterte wa Ufilipino amesaini muswada wa sheria inayoruhusu kuundwa eneo jipya lenye mamlaka ya ndani la Waislamu kusini mwa nchi hiyo.
-
Waziri Mkuu wa Tunisia akataa kujiuzulu
Jul 25, 2018 22:35Waziri Mkuu wa Tunisia amekataa ombi la Rais wa nchi hiyo aliyemtaka ajiuzulu.
-
Amnesty International yamjia juu Rais Magufuli kwa kuwadhalilisha wafungwa wa Tanzania
Jul 17, 2018 03:01Shirikisha la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limemkosoa vikali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutaka wafungwa nchini humo kufanyishwa kazi usiku na mchana na kupigwa mijeledi wakiwa wavivu.
-
Rais wa Cameroon Paul Biya kubakia madarakani hadi 2025
Jul 14, 2018 03:21Rais wa Cameroon Paul Biya, ambaye yuko madarakani kwa karibu miaka 36 sasa, ametangaza kuwa atagombea muhula mwingine katika uchaguzi wa urais wa Oktoba 7 mwaka huu.
-
Rais wa Eritrea kuitembelea Ethiopia kesho Jumamosi
Jul 13, 2018 03:21Rais wa Eritrea Isaias Afwerki anatazamiwa kuelekea nchini Ethiopia kesho Jumamosi, siku chache baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia mjini Asmara.
-
Rais wa Gambia alifanyia mabadiliko baraza la mawaziri
Jul 01, 2018 02:52Rais Adama Barrow wa Gambia amelifanyia mabadiliko baraza lake la mawaziri sanjari na kumteua makamu wake mpya.
-
Rais wa Ghana awafuta kazi wakuu wa tume ya uchaguzi
Jun 29, 2018 02:49Rais wa Ghana Nana Akufo-Addo amempiga kalamu nyekundu Mkuu wa Tume ya Uchaguzi nchini humo, Charlotte Osei kutokana kile alichotaja kama utovu wa nidhamu na utepetevu.
-
Mnangagwa ailaumu G40 inayomuunga mkono Grace Mugabe kwa mripuko
Jun 27, 2018 23:01Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema anashuku huenda kundi la G40 linalomuunga mkono Grace Mugabe, mke wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo ndilo lililohusika katika kile anachokitaja kama jaribio la mauaji dhidi yake katika mji wa Bulawayo Jumamosi iliyopita.
-
Kabila wa DRC afuata nyayo za Nkurunziza, asema hatagombea muhula wa tatu wa urais
Jun 13, 2018 02:38Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo hatagombea muhula wa tatu wa urais katika uchaguzi unaotazamiwa kufanyika baadaye mwaka huu.