-
Kukatwa kikamilifu uhusiano wa Colombia na utawala wa Kizayuni; kuendelea kutengwa Tel Aviv kimataifa
May 02, 2024 23:13Rais Gustavo Petro wa Colombia alisema siku ya Jumatano tarehe Mosi Mei katika hotuba yake kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kuwa kuanzia Alhamisi amekata kikamilifu uhusiano wa nchi hiyo na utawala wa Kizayuni kwa sababu ya jinai na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala huo huko Ukanda wa Gaza.
-
Rais wa Zambia: Tunahitaji karibu dola bilioni moja kwa ajili ya misaada ya kibinadamu
Apr 18, 2024 01:07Rais wa Zambia amesemam kuwa nchi yake inahitaji haraka Kwacha bilioni 23.5 sawa na dola milioni 937 ili kukidhi mahitaji ya haraka ya kuokoa maisha na kudhamini misaada ya kibinaamu kufuatia ukame mkubwa unaoikumba nchi hiyo.
-
Raisi: Madola ya kibeberu yanazusha fitna ili kuvuruga usalama kati ya Iran na Pakistan
Apr 12, 2024 07:48Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kustawishwa uhusiano wa Iran na Pakistan hakufurahishi madola ya kibeberu na kwa hivyo yanazusha fitna ili kuleta mpasuko kati ya mataifa hayo mawili na nchi hizo mbili za Kiislamu.
-
Raisi: Tehran yaweka katika ajenda yake ya kazi ushirikiano na nchi zote za Kiislamu
Apr 05, 2024 04:22Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika dhifa ya (futari) Iftar na mabalozi wa nchi za Kiislamu wanaoishi Tehran kwamba suala la kushirikiana na nchi zote za Kiislamu lipo katika ajenda ya utendaji ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais Museveni amteua mwanawe kuwa Mkuu wa Majeshi ya Uganda
Mar 22, 2024 07:26Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemteua mwanawe wa kiume, Jenerali Muhoozi Kainerugaba kuwa Mkuu wa Majeshi ya nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Spika wa Bunge Ghana amkosoa Rais kwa kutopasisha sheria dhidi ya LGBT
Mar 21, 2024 23:03Spika wa Bunge la Ghana, Alban Bagbin amemjia juu Rais Nana Akufo-Addo wa nchi hiyo kwa kutoidhinisha kuwa sheria muswada wa kupambana na ushoga na ubaradhuli LGBTQ+ takriban mwezi mmoja baada ya kupasishwa kwake na Bunge.
-
Joe Biden akiri kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu Marekani
Mar 17, 2024 23:03Ijumaa, Februari 15, Rais Joe Biden wa Marekani huku akikiri kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu nchini humo tangu kuanza mashambulizi ya Wazayuni huko Gaza alisema: 'Waislamu kote duniani wanapitia hali ngumu kutokana na imani yao.'
-
Rais Raisi: Uwepo wa maajinabi umelizidishia eneo hili matatizo
Feb 15, 2024 23:17Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inapinga vikali uwepo wa madola ajinabi katika eneo hili la kistratejia la Asia Magharibi.
-
Mahakama ya Juu Comoro 'yabariki' ushindi wa Rais Azali Assoumani
Jan 25, 2024 07:43Mahakama ya Juu ya Comoro imesema Rais Azali Assoumani alichaguliwa kihalali katika uchaguzi wa rais uliofanyika wiki iliyopita.
-
Raisi: Mauaji ya washauri wa kijeshi wa IRGC hayatapita bila kujibiwa
Jan 21, 2024 00:03Rais Ebrahim Raisi wa Iran amelaani vikali shambulizi la kigaidi la Israel katika mji mkuu wa Syria, Damascus lililopelekea kuuawa shahidi washauri watano wa kijeshi wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) na kusisitiza kuwa, vitendo vya aina hiyo vya kioga haviwezi kupita hivi hivi bila kupewa jibu.