-
Maana ya ushirikiano mpya wa Iran na Russia kwa ulimwengu
Jan 10, 2025 09:14Chombo kimoja cha habari cha Russia kimetathmini ushirikiano wa Iran na Russia na kuandika: Makubaliano ya pamoja ya kistratejia ni hatua muhimu katika kuimarika muungano kati ya mataifa haya mawili.
-
Vikwazo vipya vya Washington dhidi ya Iran na Russia kwa kisingizio cha kuingilia uchaguzi wa Marekani
Jan 02, 2025 08:46Wizara ya Hazina ya Marekani ilitangaza katika taarifa yake Jumanne iliyopita kuwa: "Idara ya Udhibiti wa Mali za Kigeni (OFAC) imeiwekea vikwazo taasisi tanzu ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) na shirika tanzu la Idara ya Ujasusi ya Russia (GRU) yenye makao yake makuu mjini Moscow na mkurugenzi wake.
-
Intelijensia ya Russia: US na UK zinapanga mashambulio ya kigaidi dhidi ya vituo vyetu vilivyoko Syria
Dec 29, 2024 07:33Idara ya Intelijensia ya Russia ya Nje ya Nchi (SVR) imetahadharisha kuwa Marekani na Uingereza zinapanga mashambulizi ya kigaidi katika vituo ya kijeshi vya nchi hiyo vilivyoko Syria ili hali ya nchi hiyo isitangamae na amani na uthabiti usirejee nchini humo.
-
Waasi wa ADF waua raia wasiopungua 21 mashariki ya DRC katika wiki ya Krismasi
Dec 29, 2024 07:31Waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) wameua watu wasiopungua 21 katika mashambulio kadhaa waliyofanya katika wiki ya Krismasi kwenye eneo lililokumbwa na mgogoro wa vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Baada ya Israel kuichoma moto hospitali kuu ya kaskazini ya Ghaza, yamkamata mkurugenzi na wafanyakazi wake
Dec 28, 2024 10:42Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa askari wa jeshi la utawala w Kizayuni wa Israel wamemkamata Hussam Abu Safiya, Mkurugenzi wa Hospitali ya Kamal Adwan kaskazini mwa Ghaza, na wafanyakazi wengine mapema leo, siku moja baada ya askari wa jeshi hilo kuichoma moto hospitali hiyo, ambayo ndicho kituo kikuu pekee cha afya katika eneo hilo.
-
Rais Putin wa Russia: Ninaamini Mungu. Na Mungu yu pamoja nasi
Dec 27, 2024 03:00Rais Vladimir Putin wa Russia amesema, Mungu yuko pamoja na nchi yake akionyesha kujiamini kwamba Moscow itashinda katika mzozo wake na Ukraine.
-
Russia yajibu matamshi ya Grossi kuhusu Iran: IAEA inapaswa kutoegemea upande wowote
Dec 26, 2024 06:54Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, amejibu matamshi ya Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA), akisisitiza kwamba wakala huo haupaswi kusalimu amri kwa fikira potovu za nchi za Magharibi kuhusiana na suala la Iran.
-
Makamu wa Rais wa Iran ahimiza kustawishwa uhusiano na Russia
Dec 24, 2024 03:23Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Iran amesema kuwa, viongozi wa ngazi za juu wa Iran wana nia ya kweli ya kustawisha uhusiano na Russia katika viwango vya juu.
-
Iran na Russia zahimiza kuimarishwa uhusiano wa pande mbili
Dec 23, 2024 22:59Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa, serikali yake imedhamiria kikwelikweli kuimarisha uhusiano wa Jamhuri ya Kiislamu na Russia na kukamilishwa haraka njia ya Ukanda wa Kimataifa wa Usafiri wa Kaskazini-Kusini (INSTC).
-
Onyo la Putin kuhusu kuwekwa makombora mapya ya Marekani barani Ulaya na Asia
Dec 18, 2024 07:37Rais Vladimir Putin wa Russia, ametoa onyo kuhusu kuwekwa makombora ya masafa ya kati na mafupi ya Marekani barani Ulaya na Asia, akisisitiza kwamba nchi yake itatoa jibu la pande zote kwa hatua hiyo. Putin amesema, mpango wa Washington wa kuweka makombora barani Ulaya unaitia wasiwasi mkubwa Moscow.