-
Majeshi ya Iran, Syria kushirikiana katika vita dhidi ya ugaidi
May 01, 2017 23:35Wakuu wa majeshi ya Iran na Syria wamesisitiza kuhusu kuimarisha ushirikiano wa majeshi ya nchi mbili katika vita dhidi ya ugaidi huku wakilaani vikali hujuma za Marekani na Utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Syria.
-
Marekani: Mashambulizi yetu yameua mamia ya raia Iraq na Syria
May 01, 2017 03:02Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon, imetoa taarifa na kukiri kwamba mashambulizi ya muungano unaodaiwa kupambana na magaidi wa Daesh hadi sasa yameshaua raia 352 katika nchi za Iraq na Syria tangu mwaka 2014.
-
Iran yalaani hujuma za Israel nchini Syria
Apr 29, 2017 03:10Iran imelaani vikali hujuma za mara kwa mara za kijeshi za utawala haramu wa Israel katika ardhi ya Syria na kusema lengo ni kuwapa nguvu magaidi wa kitakfiri Syria ambao wanaendelea kudhoofishwa kila siku na jeshi la nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Kuongezeka mivutano baina ya Marekani na Russia kuhusu Syria
Apr 28, 2017 22:00Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Alkhamisi jioni katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani, kimejikita kwenye hali ya kibinadamu katika nchi ya Syria iliyoharibiwa vibaya na vita.
-
Utawala haramu wa Israel hauna nafasi aktika mustakabali wa Mashariki ya Kati
Apr 28, 2017 10:10Katibu Mkuu wa Kongamano la Kimataifa la Kuunga Mkono Intifadha ya Palestina amesema: "Maadui hatimaye watasalimu amri kuhusu utatuzi wa kisiasa wa kadhia ya Syria na kwa yakini utawala haramu na wa kigaidi wa Israel hauna nafasi katika mustakabali wa Mashariki ya Kati."
-
Iran, Syria, Russia zalaani shambulizi la Israel dhidi ya uwanja wa ndege Damascus
Apr 28, 2017 03:01Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Syria na Russia zimelaani vikali shambulizi la anga lililofanywa na jeshi la utawala haramu wa Israel dhidi ya uwanja wa ndege wa Damascus jana alfajiri.
-
Wazayuni washambulia kwa makombora uwanja wa ndege Damascus, Syria
Apr 27, 2017 03:48Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya shambulizi la anga dhidi ya uwanja wa ndege wa Damascus nchini Syria, wiki tatu baada ya Marekani kutekeleza hujuma kama hiyo ya kichokozi.
-
Russia yasisitiza kuundwa muungano wa kimataifa wa kutegua mabomu huko Syria
Apr 26, 2017 08:46Russia imetaka kuundwa muungano wa kimataifa kwa ajili ya kutegua mabomu ya kutegwa ardhini huko Syria.
-
Damascus yajibu propaganda chafu za Washington kuhusu silaha za kemikali
Apr 25, 2017 00:19Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Syria amekadhibisha propaganda chafu zinazoenezwa na vyombo vya habari vya Kimarekani na kusisitiza tena kwamba Syria haina aina yoyote ya silaha za kemikali.
-
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ana imani na nafasi ya Syria katika kurejesha amani
Apr 24, 2017 06:47Antonio Guterres Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amemtumia ujumbe Rais Bashar al Assad wa Syria akimpongeza yeye na Wasyria wote kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Taifa ya nchi hiyo.