-
Bobi Wine: Nitapitia upya mikataba ya mafuta ya Uganda iwapo nitachaguliwa Rais
Jan 08, 2026 09:18Bobi Wine mgombea mkuu wa upinzani katika uchaguzi wa kiti cha urais nchini Uganda uliopangwa kufanyika wiki ijayo, amesema kuwa atapitia upya makubaliano yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na makampuni ya mafuta duniani iwapo ataibuka na ushindi. Amesema ataifanyia marekebisho mikataba yoyote ambayo haina manufaa na maslahi kwa watu wa Uganda.
-
Mgombea urais Uganda: Nilipigwa na askari usalama
Dec 07, 2025 08:49Bob Wine au Robert Kyagulanya mgombea kiti cha urais nchini Uganda kwa tiketi ya chama cha upinzani cha NUP amesema kuwa askari usalama wa nchi hiyo wampiga yeye na wafuasi wake wakati walipokuwa katika kampeni za uchaguzi kaskazini mwa nchi hiyo katika kile kinachotajwa kuwa muendelezo wa ghasia na utumiaji mabavu unaoshuhudiwa Uganda kabla ya uchaguzi wa Rais Januari 15 mwakani.
-
Uchaguzi Uganda: UN yalaani ukandamizaji dhidi ya mgombea urais wa upinzani
Dec 04, 2025 00:17Umoja wa Mataifa jana Jumatano ulikosoa kuongezeka ukandamizaji dhidi ya upinzani na vyombo vya habari nchini Uganda kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi ujao, na kutaka uchunguzi ufanyike bila upendeleo kuhusu madai ya kukamatwa raia kiholela, kutoweka na "mateso".
-
Jumanne, tarehe 11 Novemba, 2025
Nov 10, 2025 23:00Leo ni Jumanne tarehe 20 Jamadil Awwal 1447 Hijria mwafaka na tarehe 11 Disemba 2025.
-
Mahakama ya ICC yathibitisha mashtaka dhidi ya Joseph Kony
Nov 08, 2025 00:40Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC yenye makao yake mjini Hague, Uholanzi wamethibitisha kuwa kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony anakabiliwa na mashtaka ya jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu na hivyo kufungua njia kwa ajili kuanza kesi yake iwapo tu atatiwa nguvuni.
-
Watu 46 wamefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani Uganda
Oct 22, 2025 09:27Polisi ya Uganda imeripoti kuwa watu 46 wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha mabasi mawili katika barabara kuu ya Kampala kuelekea Gulu nchini humo mapema leo Jumatano.
-
Araghchi kuhudhuria mkutano wa NAM nchini Uganda
Oct 14, 2025 23:04Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu, Abbas Araghchi atazuru Uganda karibuni hivi kushiriki Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM).
-
Alkhamisi, 09 Oktoba 2025
Oct 09, 2025 09:06Leo ni Alkhamisi 16 Mfunguo Saba Rabiuthani 1447 Hijria sawa na 9 Oktoba 2025 Miladia.
-
Alkhamisi, 09 Oktoba 2025
Oct 08, 2025 23:03Leo ni Alkhamisi 16 Mfunguo Saba Rabiuthani 1447 Hijria sawa na 9 Oktoba 2025 Miladia.
-
Kampeni za uchaguzi mkuu wa Uganda wa Januari 2026 zaanza rasmi
Sep 29, 2025 08:03Kampeni za uchaguzi mkuu wa Uganda zimeanza rasmi leo Jumatatu kabla ya uchaguzi huo wa Januari 206 ambao huenda ukawa mpambano kati ya Rais aliyeko madarakani Yoweri Kaguta Museveni na mpinzani wake mkuu Robert Kyagulanyi Ssentamu, almaarufu Bobi Wine, ukitazamwa kama marudio ya uchaguzi wa 2021.