-
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu: Tunalaani aina zote za ugaidi
Jun 19, 2023 07:11Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani shambulizi la kigaidi lililoua makumi ya wanafunzi katika eneo la Mpondwe, magharibi mwa Uganda na kusisitiza kuwa, taasisi hiyo inalaani kila aina ya ugaidi.
-
Jeshi la Uganda limeanza kuwasaka wahalifu ili kuwaokoa wanafunzi waliotekwa nyara
Jun 18, 2023 06:53Uganda imeimarisha ulinzi na tayari imeanzisha msako mkubwa baada ya wanamgambo wenye silaha wa ADF wenye mfungamano na kundi la kigaidi ya Daesh (ISIS) kuwauwa watu wasiopungua 41; wengi wao wakiwa ni wanafunzi. Mauaji hayo yamefanyika katika maeneo ya Magharibi mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
UN yalaani shambulizi la kigaidi Uganda, waliouawa ni zaidi ya 40
Jun 18, 2023 04:15Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amelaani vikali shambulizi la kigaidi lililoua makumi ya wanafunzi katika eneo la Mpondwe, magharibi mwa Uganda.
-
Makumi ya wanafunzi wauawa katika hujuma ya magaidi wa ADF Magharibi mwa Uganda
Jun 17, 2023 04:28Polisi ya Uganda imetangaza kuwa, makumi ya watu wameuawa katika hujuma iliyofanywa na watu waliokuwa na silaha dhidi ya shule moja ya sekondari Magharibi mwa nchi hiyo.
-
Uganda yajibu tahadhari ya Marekani, yasema: Hatutatishwa
Jun 16, 2023 04:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda amesema taifa hilo kamwe halitasalimu amri na kukubali kuburuzwa na Marekani ili likengeuke thamani, maslahi na utamaduni wake.
-
Ethiopia yawatimua Waganda waliohadaiwa kwenda 'kuonana' na Yesu
Jun 13, 2023 03:57Mamlaka za Ethiopia zimewarejesha nyumbani raia 80 wa Uganda ambao walitapeliwa fedha zao kwa ahadi kwamba watapelekwa kukutana na Yesu katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Kanisa la Anglikana 'lasikitishwa' na sheria dhidi ya ushoga Uganda
Jun 10, 2023 07:03Kiongozi wa Kanisa la Kianglikana Duniani amedai kuwa amesikitishwa na hatua ya Uganda ya kupasisha sheria kali ya kupambana na ubaradhuli na mahusiano ya watu jinsia moja.
-
Museveni: Wanajeshi 54 wa Uganda wameuawa na al-Shabaab Somalia
Jun 04, 2023 08:02Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema makumi ya askari wa Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo (UPDF) waliuawa katika shambulio la wanamgambo wa al-Shabaab nchini Somalia wiki iliyopita.
-
Kutishiwa kuwekewa vikwazo Uganda, njama za Marekani za kuzitwisha ufuska nchi za Afrika
Jun 01, 2023 08:42Rais wa Marekani, Joe Biden amelaani sheria mpya iliyotiwa saini na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda dhidi ya vitendo vya ushoga na kusema kuwa Marekani inaweza kuiwekea Uganda vikwazo na ameitaka Uganda kufuta mara moja sheria hiyo.
-
Sheria dhidi ya LGBTQ Uganda yamkasirisha rais wa Marekani, atishia kuiwekea nchi hiyo vikwazo
May 30, 2023 03:11Rais Joe Biden wa Marekani amelaani sheria mpya iliyotiwa saini na Rais Yoweri Museveni wa Uganda dhidi ya vitendo vya ushoga na kusema kuwa Marekani inaweza kuiwekea Uganda vikwazo huku akitoa wito wa sheria hiyo kufutwa mara moja.