-
Ughali wa maisha Uingereza: Wafanyakazi wa usalama wa Heathrow wagoma
Apr 01, 2023 22:59Wafanyikazi wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Heathrow mjini London nchini Uingereza wameanzisha mgomo wa siku 10, wakiungana na wafanyakazi wengine wa serikali na wafanyikazi wa sekta kadhaa nchini humo ambao wamegoma wakitaka nyongeza kubwa ya mishahara kutokana na mfumuko wa bei unaozidi kuongezeka.
-
Netanyahu akaribishwa UK kwa maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina
Mar 25, 2023 04:36Mamia ya waungaji mkono wa Palestina na wapinzani wa utawala haramu wa Israel wamefanya maandamano mjini London, kulaani safari ya Waziri Mkuu wa utawala huo wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu nchini Uingereza.
-
Marubani wa Israel wakataa kumpeleka Netanyahu Uingereza
Mar 24, 2023 03:35Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel amelazimika kuakhirisha safari yake ya kuitembelea Uingereza, baada ya marubani kadhaa wa utawala huo kukataa kumsafirisha kwa ndege katika nchi hiyo ya Ulaya mtawala huyo mwenye misimamo mikali.
-
Botswana yatishia kukata uhusiano na kampuni ya almasi ya Uingereza
Feb 13, 2023 06:47Rais Mokgweetsi Masisi wa Botswana ameonya kuwa, huenda nchi yake ikavunja uhusiano na shirika kubwa la kimataifa la almasi la De Beers, lenye makao yake huko London, Uingereza, kwa kupunjwa.
-
Sana'a: Uingereza sababu kuu ya uvamizi Yemen
Jan 22, 2023 07:48Waziri Mkuu wa Serikali ya Uokovu wa Kitaifa ya Yemen ameeleza kuwa, Uingereza si tu haiwezi kusaidia kupunguza mateso na masaibu ya kiuchumi ya wananchi wa Yemen bali nchi hiyo ni sehemu kuu ya njama ya kuvamiwa nchi hiyo.
-
Radiamali hasi ya Madola ya Magharibi ya kunyongwa jasusi wa Uingereza nchini Iran
Jan 15, 2023 08:13Kunyongwa Ali Reza Akbari, jasusi wa shirika la kijasusi la Uingereza la MI6 kumekabiliwa na matamshi ya pupa na radiamali tofauti na hasi za madola ya Magharibi. Radiamali hizo zinaonyesha kupata pigo kubwa mipango ya kijasusi ya Magharibi dhidi ya Iran.
-
UK yamuita nyumbani balozi wake baada ya Iran kumnyonga jasusi wa MI6
Jan 15, 2023 03:39Katika hatua nyingine ya uingiliaji kati wa mambo, London imemuita nyumbani balozi wa Uingereza mjini Tehran eti kwa ajili ya mashauriano, kufuatia hatua ya Idara ya Mahakama ya Iran kumnyonga Ali Reza Akbari, aliyekuwa jasusi wa shirika la kijasusi la Uingereza la MI6.
-
Fedheha! Uingereza yashindwa kutuma satalaiti yake anga za mbali
Jan 10, 2023 04:00Jaribio la Uingereza la kuwa nchi ya kwanza ya Ulaya kurusha satalaiti katika anga za mbali limegonga mwamba, huku kampuni ya Virgin Orbit ikitangaza kuwa roketi lake la kurushia satalaiti hiyo lilikubwa na hitilafu na kuifanya (satalaiti hiyo) ishindwe kufika katika anga za mbali.
-
Wataalamu: Ukoloni wa Uingereza ulisababisha vifo vya mamilioni ya watu nchini India
Dec 28, 2022 00:51Ukoloni wa Uingereza ulikuwa sababu ya vifo vya zaidi ya watu milioni mia moja nchini India.
-
Wauguzi UK wagoma wakitaka nyongeza ya mshahara
Dec 15, 2022 22:56Wauguzi wapatao laki moja kote nchini Uingereza wameanza mgomo kushinikiza malipo bora na mazingira mazuri ya kazi.