-
Katibu Mkuu wa UN aonya: Kikosi kitakachotumwa Ghaza lazima kiwe na "uhalali kamili wa kimataifa"
Nov 05, 2025 23:50Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonya kuwa kikosi chochote cha kurejesha uthabiti na utulivu kitakachopelekwa Ukanda wa Ghaza lazima kiwe na "uhalali kamili wa kimataifa" ili kuwasaidia Wapalestina wa eneo hilo.
-
UNICEF: Usitishaji vita Gaza ni fursa muhimu ya kukidhi mahitaji ya watoto
Oct 27, 2025 23:44Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaweza kuwa "fursa muhimu" ya kulinda maisha, utu na mahitaji muhimu ya watoto milioni moja wa Kipalestina.
-
Malori ya misaada 986 tu kati ya 6,600 yameingia Gaza tangu kufikiwa makubaliano ya kusitisha vita
Oct 22, 2025 09:39Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Serikali ya Gaza imeripoti kuwa ni malori 986 pekee ya misaada yaliyoingia katika eneo hilo linalozingirwa tangu kusitishwa kwa mapigano kati ya Harakati ya Mapambano ya Palestina (Hamas) na utawala wa Israel tarehe 10 mwezi huu.
-
Hamas: Israel lazima igharamie ujenzi mpya wa Gaza
Oct 21, 2025 08:01Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, Mousa Abu Marzouk ametoa wito kwa Israel kufadhili kikamilifu ukarabati na ujenzi mpya wa Ukanda wa Gaza, akitaja uharibifu mkubwa na haki za Wapalestina zaidi ya milioni mbili ambao wamepoteza makazi yao, makazi na riziki.
-
Iran yailaani Israel kwa kuendelea kuua wanawake na watoto Gaza
Oct 19, 2025 03:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amelaani ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, likiwemo shambulio la hivi karibuni dhidi ya gari lililokuwa limebeba familia ya Kipalestina wakati ikirejea kwenye makazi yao.
-
Malori ya misaada yasubiri 'idhini ya Israel' Rafah ili yaingie Gaza
Oct 16, 2025 01:54Gavana wa Sinai Kaskazini nchini Misri amesema mamia ya malori ya misaada yapo tayari kuingia katika Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha Rafah, lakini yanasubiri kibali cha utawala wa Israel ili yaingize misaada hiyo ya dharura.
-
Israel yaua Wapalestina wengine 6 huko Gaza; Hamas yalalamikia kukiukwa usitishaji vita
Oct 14, 2025 09:23Jeshi la Israel limewauwa shahidi takriban Wapalestina sita huko Ukanda wa Gaza ndani ya saa 24, licha ya Tel Aviv hivi karibuni kufikia makubalianokuhusu utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango wa kusitisha vita.
-
HAMAS: Tony Blair hakaribishwi kuwa na nafasi yoyote katika uongozi wa Ghaza baada ya vita
Oct 12, 2025 02:14Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imeonya kwamba Tony Blair hatakaribishwa kuwa na nafasi yoyote ya uendeshaji wa Ghaza kufuatia kuanza kutekelezwa usitishaji vita katika eneo hilo la Palestina.
-
"Israel haiaminiki; Iran inaunga mkono kusimamishwa mauaji ya kimbari Gaza"
Oct 11, 2025 23:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesema Jamhuri ya Kiislamu inakaribisha kusitishwa kwa mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza, huku akitoa indhari juu ya tabia ya kutokuwa na muamana Tel Aviv kwa kukiuka makubaliano kadhaa ya huko nyuma.
-
Iran: Tunaunga mkono mpango wowote wa kumaliza vita, mauaji ya kimbari Gaza
Oct 09, 2025 23:51Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba Jamhuri ya Kiislamu daima inaunga mkono mpango wowote unaolenga kukomesha vita na mauaji ya halaiki huko Gaza, na kusisitiza ulazima wa kuwa macho mkabala wa hulka ya utawala wa Israel ya kukiuka ahadi na makubaliano.