-
Umoja wa Mataifa watoa onyo kali kuhusu kuongezeka majanga katika Ukanda wa Gaza
Jun 21, 2024 02:14Francesca Albanese, Ripota wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Palestina, amesema katika taarifa kwamba hali ya maafa huko Ukanda wa Gaza imezidi kuwa mbaya. Kwa kauli yake, utawala haramu wa Israel unalenga misafara ya misaada ya kibinadamu inayotumwa Gaza na kuzuia ufikaji wa misaada katika ukanda huo.
-
Martin Griffiths : Upuuzaji wa Israel hauwezi kuendelea; ataka kulindwa raia
May 28, 2024 07:54Mratibu mkuu wa misaada na masuala ya dharura wa Umoja wa Mataifa amelaani mashambulizi ya utawala wa Israel katika kambi ya wakimbizi wa ndani wa Kipalestina katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza akisema kuwa upuuzaji wa Israel hauwezi kuendelea. Afisa huyo wa Umoja wa Mataifa ametaka kulindwa raia na kuruhusiwa kuelekea maeneo salama.
-
UN yaitaka Israel isimamishe mashambulio Rafah kama ilivyoagizwa na ICJ
May 25, 2024 11:06Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameutaka utawala haramu wa Israel uheshimu na utekeleza amri ya kusitisha operesheni za kijeshi mjini Rafah, kama ilivyoagizwa na mahakama kuu ya Umoja wa Mataifa.
-
Ripota Maalumu wa UN ataka Israel iwekewe vikwazo
May 25, 2024 11:02Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ametoa mwito wa kuwekewa vikwazo utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Guterres: Afrika ina mchango muhimu kwa amani na usalama wa dunia
May 24, 2024 07:22Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameashiria nafasi muhimu ya Afrika katika kuufanya ulimwengu uwe pahala pazuri na salama na kusisitiza kuwa, "Wakati umefika wa kuanika uwezo wa amani wa Afrika."
-
TZ yaitoa hofu UNHCR: Hatutafunga kambi wala kuwalazimisha wakimbizi warudi makwao
May 23, 2024 07:19Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limesema limepewa hakikisho na Serikali ya Tanzania kwamba kambi ya wakimbizi ya Nduta inayowapa hifadhi wakimbizi wa Burundi haitafungwa na wala wakimbizi hao hawatalazimishwa kurudi makwao.
-
UN: 40% ya wakazi wa Gaza wamelazimika kuhama makwao ndani ya wiki 2
May 21, 2024 07:19Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadu (OCHA) imesema asilimia 40 wa Wapalestina wa Ukanda wa Gaza wamelazimika kuyahama makazi yao katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.
-
OCHA: Kwa kuzuiwa uingizaji misaada, hakuna kilichobaki kugawa katika Ukanda wa Ghaza
May 19, 2024 02:48Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imeonya dhidi ya kuzuiwa uingizaji misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza na kutangaza kuwa hakuna kilichosalia kwa ajili ya kuwagaia Wapalestina wa eneo hilo.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani mauaji ya wafanyakazi wa afya huko Rafah
May 15, 2024 06:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amelaani mauaji na kujeruhiwa kwa maafisa wa afya wa Umoja wa Mataifa huko Rafah kusini mwa ukanda wa Gaza.
-
Kuidhinishwa rasimu ya uanachama kamili wa Palestina katika Umoja wa Mataifa
May 11, 2024 11:21Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) hatimaye limeipigia kura ya ndio rasimu ya uanachama kamili wa Palestina katika umoja huo baada ya Marekani kukwamisha suala hilo kwa miaka kadhaa.