-
Sisitizo kwa Umoja wa Ulaya la kujitoa katika makucha ya Marekani
Jan 26, 2018 00:29Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, amesema mbele ya Baraza la Kimataifa la Uchumi mjini Davos Uswisi kwamba nchi za Ulaya zinapaswa kubadilisha siasa zao za kuitegemea Marekani katika masuala ya ndani na nje ya bara hilo.
-
Mogherini: Umoja wa Ulaya utaendelea kuheshimu maafikiano ya nyuklia ya JCPOA
Jan 11, 2018 12:56Mkuu wa Siasa za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, umoja huo umeamua kuheshimu maafikiano ya nyuklia ya JCPOA.
-
EU kufanya mkutano wa dharura wa wafadhili wa Palestina
Jan 11, 2018 04:21Umoja wa Ulaya na Norway zinatazamiwa kufanya kikao cha dharura cha nchi wafadhili wa Palestina karibuni hivi, baada ya Marekani kutishia kuikatia misaada taasisi ya Umoja wa Mataifa inayoshuughulikia wakimbizi wa Kipalestina.
-
EU: Uchaguzi wa Kenya ulizungukwa na ufisadi na vitisho
Jan 10, 2018 12:43Mkuu wa timu ya waangalizi wa Umoja wa Ulaya katika uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti na Oktoba mwaka uliomalizika 2017 nchini Kenya amesema kampeni zilizotangulia zoezi hilo ziligubikwa na rushwa, utumiaji wa mali za umma na vitisho.
-
Watu 15,000 wanakuwa wakimbizi kila siku barani Afrika
Jan 07, 2018 00:26Taasisi moja ya barani Ulaya inayoshughulikia masuala ya wakimbizi imetangaza kuwa, katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Juni mwaka jana 2017, kila siku watu 15,000 walikuwa wakikimbia makazi yao barani Afrika.
-
Erdogan: Uturuki imechoka kusubiri kujumuishwa EU
Jan 06, 2018 04:13Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema Waturuki wamechoka kusubiri kujua iwapo nchi yao itajumuishwa kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya au la.
-
Umoja wa Ulaya wakosoa ukandamizaji wa serikali ya Congo DR dhidi ya wapinzani
Jan 03, 2018 23:43Umoja wa Ulaya umewatuhumu maafisa wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuwa wanakabiliana kwa mabavu na matakwa ya wananchi wanaosisitiza udharura wa kuondoka madarakani rais wa sasa wa nchi hiyo.
-
EU: Tumeandaa mpango maalumu wa kuwaondoa wahajiri 15 elfu nchini Libya
Dec 15, 2017 00:48Mkuu wa Siasa za Kigeni za Umoja wa Ulaya amesema kuwa umoja huo umeandaa mpango maalumu wa kuwaondoa wahajiri 15 wa Kiafrika kutoka katika ardhi ya Libya.
-
Amnesty yasema EU inashiriki katika kuteswa wahajiri Libya
Dec 12, 2017 04:45Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limezituhumu nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya kuwa zinashiriki katika kuteswa, kukandamizwa na kudhalilishwa wahajiri wanaozuiliwa nchini Libya.
-
Radiamali ya Umoja wa Ulaya kuhusu hatua ya Trump dhidi ya Quds Tukufu
Dec 08, 2017 01:18Federica Mogherini, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amelaani hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kutambua rasmi mji wa Beitul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel na kuongeza kuwa hatua hiyo ya upande mmoja bila shaka itavuruga utulivu wa ulimwengu na juhudi zote zilizofanywa kwa ajili ya kutatua mzozo wa Palestina.