-
Wasia wa ripota Mpalestina aliyeuliwa kigaidi na Israel kwa walimwengu: 'Msiisahau Ghaza'
Aug 11, 2025 10:49Anas al-Sharif, ripota mashuhuri wa chaneli ya Al Jazeera aliyeuliwa shahidi pamoja na wenzake wanne katika shambulio la makusudi lililofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel kwenye hema la waandishi wa habari katika Mji wa Ghaza, amewaomba walimwengu katika wasia wake wasiisahau Ghaza iliyowekewa mzingiro pamoja na watu wa Palestina.
-
Katika muda wa juma moja, watu 63 wameaga dunia kwa lisheduni mjini El-Fasher, Sudan
Aug 11, 2025 10:49Watu wasiopungua 63, wengi wao wakiwa wanawake na watoto wamefariki dunia kutokana na upungufu wa lishe katika mji uliozingirwa wa El-Fasher, makao makuu ya jimbo la Darfur Kaskazini nchini Sudan.
-
Watu zaidi ya 530 watiwa nguvuni London kwa kuiunga mkono Palestina
Aug 11, 2025 09:06Polisi ya London imetangaza kuwa jumla ya waandamanaji 532 wametiwa mbaroni wakati wa maandamano ya kuunga mkono kundi linalojulikana kwa jina la Palestine Action Group linalowatetea Wapalestina.
-
Afrika Kusini yasisitiza tena msimamo wake kuhusu mauaji ya kimbari ya Israel, Gaza
Aug 10, 2025 09:22Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini kwa mara nyingine tena amesisitiza kuhusu msimamo wa nchi hiyo katika faili la kesi ya mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni huko Gaza na kusema: Afrika Kusini inaitaka Israel isimamishe vita haraka iwezekanavyo huko Gaza, iruhusu misaada ya kibinadamu kuingia katika eneo hilo, iache kulikalia kwa mabavu eneo hilo na iache kuiaadhibu jamii ya Wapalestina.
-
Venezuela yalaani uamuzi wa utawala wa Kizayuni wa kuukalia kwa mabavu Ukanda wa Gaza
Aug 09, 2025 13:30Serikali ya Venezuela imepinga vikali mpango wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuukalia kwa mabavu Ukanda wa Gaza na kuitaja hatua hiyo kuwa ni kuzidisha mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Palestina.
-
UEFA yamuenzi 'Pele wa Palestina' aliyeuliwa na jeshi la Israel Ghaza wakati anangojea chakula
Aug 09, 2025 07:41Muungano wa Vyama vya Soka vya Ulaya UEFA, umemuenzi nahodha na nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Palestina Suleiman al-Obeid, ambaye aliuawa shahidi katika shambulizi la kinyama la utawala wa kizayuni wa Israel alipokuwa akisubiri msaada wa chakula huko Ghaza siku ya Jumatano.
-
Mbunge wa Hizbullah: Kukubali tupokonywe silaha ni sawa na kujinyonga
Aug 09, 2025 07:22Mbunge wa Lebanon kutoka mrengo wa kisiasa wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya nchi hiyo Hizbullah amelipinga vikali dai la kuitaka harakati hiyo iweke chini silaha zake kufuatia shinikizo la Marekani kwa serikali la kuitaka iipokonye silaha harakati hiyo.
-
Israel yasaini makubaliano ya kihistoria ya kuiuzia Misri gesi yenye thamani ya dola bilioni 35
Aug 09, 2025 06:57Utawala wa kizayuni wa Israel umetangaza kusainiwa mkataba mkubwa utakaogharimu dola bilioni 35 wa kuiuzia Misri gesi asilia, unaotajwa kuwa ni "mkubwa zaidi katika historia ya Israel". Hayo yameelezwa na Eli Cohen, waziri wa nishati wa utawala huo ghasibu.
-
Serikali ya Chad yaomba waziri mkuu wa zamani apewe adhabu ya kifungo cha miaka 25 jela
Aug 09, 2025 06:57Serikali ya Chad imeiomba mahakama impe adhabu ya kifungo cha muda mrefu jela waziri mkuu wa zamani Succes Masra ambaye anakabiliwa na mashtaka yanayohusiana namachafuko mabaya yaliyozuka kusini mwa nchi hiyo mwezi Mei mwaka huu na kusababisha vifo vya makumi ya watu.
-
Kwa nini India inashirikiana na utawala wa kizayuni wa Israel?
Aug 09, 2025 02:29Katika miaka ya hivi karibuni India na utawala wa Kizayuni zimeanzisha uhusiano mkubwa katika sekta nyingi za kiuchumi, kijeshi na kisiasa.