-
UN: Waislamu wa Rohingya walioko Bangladesh hawataki kurejea Myanmar
Aug 20, 2019 22:10Maafisa wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) na wale wa serikali ya Bangladesh wametangaza kuwa, Waislamu wa jamii ya Rohingya waliokimbilia nchini Bangladesh hawataki kurejea katika nchi yao ya Myanmar.
-
Waziri Mkuu wa Pakistan atahadharisha kuhusu uwezekano wa kutokea vita na India
Aug 07, 2019 03:30Waziri Mkuu wa Pakistan ametahadharisha kuwa, kuna uwezekano wa kutokea vita baina ya nchi yake na India baada ya New Delhi kufuta kifungu cha katiba kinacholipa mamlaka ya utawala wa ndani jimbo linalozozaniwa na Kashmir.
-
Kwa nini Imarati imeamua kupunguza idadi ya wanajeshi wake huko Yemen?
Jun 29, 2019 23:46Baadhi ya duru za habari zimeripoti kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) umepunguza idadi ya askari wake waliokuwa katika mji wa Aden huko kusini mwa Yemen.
-
Marekani imechanganyikiwa katika sera zake kuhusu Iran
Jun 24, 2019 03:34Utawala wa Marekani unaendelea kuchanganyikiwa katika sera zake kuhusu Iran na hali hiyo ilifikia kilele chake baada ya ndege isiyo na rubani (drone) ya kijasusi ya Marekani kutunguliwa na vikosi vya kijeshi vya Iran Alhamisi iliyopita.
-
Zarif: Timu B ilijaribu kumtia mtegoni Trump aingie katika vita na Iran
Jun 23, 2019 23:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema tukio la hivi karibuni la drone ya Marekani kukiuka anga ya Iran katika Bahari ya Oman ilikuwa sehemu ya njama pana za wapenda vita (Timu B) kumtia mtegoni Rais Donald Trump wa Marekani ili aingie katika vita na Iran.
-
UN: Vita vimewafanya watu milioni 71 duniani kuwa wakimbizi
Jun 19, 2019 03:09Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limesema takriban watu milioni 71 wamelazimika kuwa wakimbizi kutokana na vita na mapigano katika kona mbalimbali za dunia.
-
Indhari ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali inavyozidi kuwa mbaya nchini Libya
May 23, 2019 03:43Kuendelea vita nchini Libya kumezidisha machafuko na mgogoro katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kiasi kwamba Ghassan Salamé, mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya amesema katika ripoti yake ya hivi karibuni kabisa kwamba, hatoi tahadhari kuhusu kutokea vita vya ndani na vya umwagaji damu tu, bali anatoa onyo la kusambaratika vipande vipande Libya.
-
Libya katika ncha ya kutumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe
May 22, 2019 03:26Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya ameonya kuwa, taifa hilo lenye utajiri wa mafuta liko katika ncha ya kutumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vitaigawa nchi hiyo mapande mapande.
-
Kamanda wa IRGC: Iran haitaki vita, lakini pia haiogopi vita
May 19, 2019 10:00Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Meja Jenerali Hussein Salami amesema kuwa Iran haitaki vita lakini pia wakati huo huo haiogopi vita.
-
Iran yasema vita havitaibuka katika eneo
May 19, 2019 03:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammad Javad Zarif amesema hakuna vita vitakavyoibuka Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) pamoja na kuwepo hali ya taharuki baina ya Iran na Marekani.